< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
`To the ouercomere; leese thou not the salm of the song of Asaph. God, we schulen knouleche to thee, `we schulen knouleche; and we schulen inwardli clepe thi name.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
We schulen telle thi merueilis; whanne Y schal take tyme, Y schal deme riytfulnesses.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
The erthe is meltid, and alle that duellen ther ynne; Y confermede the pileris therof.
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I seide to wickid men, Nyle ye do wickidli; and to trespassouris, Nyle ye enhaunce the horn.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Nyle ye reise an hiy youre horn; nyle ye speke wickidnesse ayens God.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For nether fro the eest, nethir fro the west, nethir fro desert hillis; for God is the iuge.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
He mekith this man, and enhaunsith hym; for a cuppe of cleene wyn ful of meddling is in the hoond of the Lord.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
And he bowide of this in to that; netheles the drast therof is not anyntischid; alle synneris of erthe schulen drinke therof.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
Forsothe Y schal telle in to the world; Y schal synge to God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
And Y schal breke alle the hornes of synneris; and the hornes of the iust man schulen be enhaunsid.

< Zaburi 75 >