< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
To the chief Musician, Al-taschith, A Psalm [or] Song of Asaph. To thee, O God, do we give thanks, [to thee] do we give thanks: for [that] thy name is near, thy wondrous works declare.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
When I shall receive the congregation I will judge uprightly.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
The earth and all its inhabitants are dissolved: I bear up the pillars of it. (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I said to the fools, Deal not foolishly; and to the wicked, Lift not up the horn:
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Lift not up your horn on high: speak [not with] a stiff neck.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For promotion [cometh] neither from the east, nor from the west, nor from the south.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
But God [is] the judge: he putteth down one, and setteth up another.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
For in the hand of the LORD [there is] a cup, and the wine is red; it is full of mixture, and he poureth out of the same: but the dregs of it all the wicked of the earth shall wring [them] out, [and] drink [them].
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
But I will declare for ever; I will sing praises to the God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
All the horns of the wicked also will I cut off; [but] the horns of the righteous shall be exalted.

< Zaburi 75 >