< Zaburi 75 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
to/for to conduct Do Not Destroy Do Not Destroy melody to/for Asaph song to give thanks to/for you God to give thanks and near name your to recount to wonder your
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
for to take: recieve meeting: time appointed I uprightness to judge
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
to melt land: country/planet and all to dwell her I to measure pillar her (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
to say to/for to be foolish not to be foolish and to/for wicked not to exalt horn
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
not to exalt to/for height horn your to speak: speak in/on/with neck arrogant
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
for not from exit and from west and not from wilderness to exalt
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
for God to judge this to abase and this to exalt
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
for cup in/on/with hand LORD and wine to aggitate full mixture and to pour from this surely dreg her to drain to drink all wicked land: country/planet
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
and I to tell to/for forever: enduring to sing to/for God Jacob
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
and all horn wicked to cut down/off to exalt horn righteous