< Zaburi 75 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
For the leader; al tashheth. A psalm of Asaph, a song. We praise you, God, we praise you: we would call on your name and declare your wonders.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
“At the time I choose, I will judge fairly.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
Though earth melt and all her inhabitants, it is I who keep steady her pillars.” (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I say to the boasters, “Boast not”; to the wicked, “Lift not up your horn:
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
lift not your horn on high, speak not boldly against the Rock.”
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For not from east nor west, not from desert nor mountains;
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
but God himself is the judge, humbling one and exalting another.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
In the hand of the Lord is a cup foaming wine, richly spiced. Out of this he pours a draught, and all the wicked of earth must drain it down to the dregs.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
But I will rejoice forever, singing praise to the God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
I will hew all the horns of the wicked, but the horns of the just shall be lifted.