< Zaburi 75 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
For the end, Destroy not, a Psalm of a Song for Asaph. We will give thanks to you, O God, we will give thanks, and call upon your name: I will declare all your wonderful works.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
When I shall take a set time, I will judge righteously.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
The earth is dissolved, and all that dwell in it: I have strengthened its pillars. (Pause)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I said to the transgressors, Do not transgress; and to the sinners, Lift not up the horn.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Lift not up your horn on high; speak not unrighteousness against God.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For [good comes] neither from the east, nor from the west, nor from the desert mountains.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
For God is the judge; he puts down one, and raises up another.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
For [there is] a cup in the hand of the Lord, full of unmingled wine; and he has turned [it] from side to side, but its dregs have not been wholly poured out; all the sinners of the earth shall drink [them].
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
But I will exult for ever: I will sing praises to the God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
And I will break all the horns of sinners; but the horns of the righteous one shall be exalted.