< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
For the Leader; Al-tashheth. A Psalm of Asaph, a Song. We give thanks unto Thee, O God, we give thanks, and Thy name is near; men tell of Thy wondrous works.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
'When I take the appointed time, I Myself will judge with equity.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
When the earth and all the inhabitants thereof are dissolved, I Myself establish the pillars of it.' (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I say unto the arrogant: 'Deal not arrogantly'; and to the wicked: 'Lift not up the horn.'
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Lift not up your horn on high; speak not insolence with a haughty neck.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For neither from the east, nor from the west, nor yet from the wilderness, cometh lifting up.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
For God is judge; He putteth down one, and lifteth up another.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
For in the hand of the LORD there is a cup, with foaming wine, full of mixture, and He poureth out of the same; surely the dregs thereof, all the wicked of the earth shall drain them, and drink them.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
But as for me, I will declare for ever, I will sing praises to the God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
All the horns of the wicked also will I cut off; but the horns of the righteous shall be lifted up.

< Zaburi 75 >