< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
To the chief Musician. 'Destroy not.' A Psalm of Asaph: a Song. Unto thee we give thanks, O God, we give thanks; and thy name is near: thy marvellous works declare it.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
When I shall receive the assembly, I will judge with equity.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
The earth and all the inhabitants thereof are dissolved: I have established its pillars. (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I said unto the boastful, Boast not; and to the wicked, Lift not up the horn:
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Lift not up your horn on high; speak not arrogantly with a [stiff] neck.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For not from the east nor from the west, nor yet from the south doth exaltation [come]:
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
For God is the judge; he putteth down one and exalteth another.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
For in the hand of Jehovah there is a cup, and it foameth with wine, it is full of mixture; and he poureth out of the same; yea, the dregs thereof shall all the wicked of the earth drain off, [and] drink.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
But as for me, I will declare for ever; I will sing psalms to the God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
And all the horns of the wicked will I cut off; [but] the horns of the righteous shall be exalted.

< Zaburi 75 >