< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
We give thanks to thee, O God. We give thanks, for thy name is near. Men tell of thy wondrous works.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
When I shall find the set time, I will judge uprightly;
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
when the earth and all the inhabitants thereof are dissolved. I have set up the pillars of it. (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
I said to the arrogant, Deal not arrogantly, and to the wicked, Lift not up the horn.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Lift not up your horn on high. Speak not with a stiff neck.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
For neither from the east, nor from the west, nor yet from the south, comes lifting up.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
But God is the judge. He put one down, and lifts another up.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
For in the hand of Jehovah there is a cup, and the wine foams. It is full of mixture, and he pours out of the same, surely to the dregs of it. All the wicked of the earth shall drain them, and drink them.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
But I will declare forever. I will sing praises to the God of Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
All the horns of the wicked I will also cut off, but the horns of a righteous man shall be lifted up.

< Zaburi 75 >