< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Salmo de Asaf. Ciertamente bueno es Dios a Israel, a los limpios de corazón.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
En cuanto a mí, casi se apartaron mis pies; por poco resbalaron mis pasos.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Porque me enojé contra los locos, viendo la paz de los impíos.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Porque no hay ataduras para su muerte; antes su fortaleza está entera.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
No pasan trabajos como otros seres humanos; ni son azotados con los hombres.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Por tanto, la soberbia los corona; se cubren de vestido de violencia.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Sus ojos están salidos de gruesos; logran con creces los antojos del corazón.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Se soltaron, y hablan con maldad de hacer violencia; hablan con altanería.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Ponen contra el cielo su boca, y su lengua pasea la tierra.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Por eso su pueblo volverá aquí, y aguas de lleno le son exprimidas.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Y dirán: ¿Cómo sabe Dios? ¿Y hay conocimiento en lo más alto?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
He aquí estos impíos, sin ser turbados del mundo, alcanzaron riquezas.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Verdaderamente en vano he limpiado mi corazón, y lavado mis manos en limpieza;
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
y he sido azotado todo el día, y castigado por las mañanas:
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Si dijera yo, hablaré como ellos; he aquí habría negado la generación de tus hijos:
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Pensaré pues para entender esto; es a mis ojos duro trabajo.
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Hasta que venga al santuario de Dios, entonces entenderé la postrimería de ellos.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Ciertamente los has puesto en deslizaderos; en asolamientos los harás caer.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
¡Cómo han sido asolados! ¡Cuán en un punto! Se acabaron, fenecieron con turbaciones.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Como sueño del que despierta, así, Señor, cuando despertares, menospreciarás sus apariencias.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Se desazonó a la verdad mi corazón, y en mis riñones sentía punzadas.
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Mas yo era ignorante, y no entendía; era como una bestia acerca de ti.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Con todo, yo siempre estuve contigo; trabaste de mi mano derecha.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Me has guiado según tu consejo, y después me recibirás con gloria.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
¿A quién tengo yo en los cielos sino a ti? Y fuera de ti nada deseo en la tierra.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Mi carne y mi corazón desfallecen; la fuerza de mi corazón es que mi porción es Dios para siempre.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Porque he aquí, los que se alejan de ti perecerán; tú cortas a todo aquel que fornica de ti.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Y en cuanto a mí, el acercarme a Dios me es el bien; he puesto en el Señor DIOS mi esperanza, para contar todas tus obras.

< Zaburi 73 >