< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Un salmo de Asaf. Ciertamente Dios es bueno con Israel, a los puros de corazón.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Pero en cuanto a mí, mis pies estaban casi perdidos. Mis pasos estuvieron a punto de resbalar.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Porque tuve envidia de los arrogantes, cuando vi la prosperidad de los malvados.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Porque no hay luchas en su muerte, pero su fuerza es firme.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Están libres de las cargas de los hombres, ni están plagados como los demás hombres.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Por eso el orgullo es como una cadena alrededor de su cuello. La violencia los cubre como una prenda.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Sus ojos están llenos de grasa. Sus mentes sobrepasan los límites de la presunción.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Se burlan y hablan con malicia. En la arrogancia, amenazan con la opresión.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Han puesto su boca en los cielos. Su lengua camina por la tierra.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Por eso su pueblo vuelve a ellos, y beben agua en abundancia.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Dicen: “¿Cómo lo sabe Dios? ¿Hay conocimiento en el Altísimo?”
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
He aquí, estos son los malvados. Estando siempre a gusto, aumentan sus riquezas.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Seguramente he limpiado mi corazón en vano, y me lavé las manos con inocencia,
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Porque todo el día he estado atormentado, y castigado cada mañana.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Si hubiera dicho: “Voy a hablar así”, he aquí que habría traicionado a la generación de tus hijos.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Cuando traté de entender esto, era demasiado doloroso para mí...
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
hasta que entré en el santuario de Dios, y consideró su último fin.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Seguramente los pusiste en lugares resbaladizos. Los arrojas a la destrucción.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
¡Cómo se destruyen de repente! Están completamente arrastrados por los terrores.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Como un sueño cuando uno se despierta, así que, Señor, cuando despierte, despreciará sus fantasías.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Porque mi alma se afligió. Estaba amargado en mi corazón.
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Era tan insensible e ignorante. Yo era una bestia bruta antes de ti.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Sin embargo, yo estoy continuamente con vosotros. Has sostenido mi mano derecha.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Me guiarás con tu consejo, y después recibirme en la gloria.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
¿A quién tengo en el cielo? No hay nadie en la tierra a quien desee además de ti.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Mi carne y mi corazón fallan, pero Dios es la fuerza de mi corazón y mi porción para siempre.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Porque, he aquí, los que están lejos de ti perecerán. Has destruido a todos los que te son infieles.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Pero me conviene acercarme a Dios. He hecho del Señor Yahvé mi refugio, para que pueda contar todas tus obras.

< Zaburi 73 >