< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Коль благ Бог Израилев правым сердцем.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Мои же вмале не подвижастеся нозе: вмале не пролияшася стопы моя:
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
яко возревновах на беззаконныя, мир грешников зря:
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
яко несть восклонения в смерти их и утверждения в ране их:
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
в трудех человеческих не суть, и с человеки не приимут ран.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Сего ради удержа я гордыня их до конца: одеяшася неправдою и нечестием своим.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Изыдет яко из тука неправда их: преидоша в любовь сердца.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Помыслиша и глаголаша в лукавстве, неправду в высоту глаголаша:
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
положиша на небеси уста своя, и язык их прейде по земли.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Сего ради обратятся людие Мои семо, и дние исполнени обрящутся в них.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
И реша: како уведе Бог? И аще есть разум в Вышнем?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Се, сии грешницы и гобзующии в век удержаша богатство.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
И рех: еда всуе оправдих сердце мое и умых в неповинных руце мои,
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
и бых язвен весь день, и обличение мое на утрених?
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Аще глаголах, повем тако: се, роду сынов Твоих, емуже обещахся:
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
и непщевах разумети: сие труд есть предо мною,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
дондеже вниду во святило Божие и разумею в последняя их.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Обаче за льщения их положил еси им злая, низложил еси я, внегда разгордешася.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Како быша в запустение? Внезапу изчезоша, погибоша за беззаконие свое.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Яко соние востающаго, Господи, во граде Твоем образ их уничижиши.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Яко разжжеся сердце мое, и утробы моя изменишася:
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
и аз уничижен, и не разумех, скотен бых у Тебе.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
И аз выну с Тобою: удержал еси руку десную мою,
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
и советом Твоим наставил мя еси, и со славою приял мя еси.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Что бо ми есть на небеси? И от Тебе что восхотех на земли?
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Изчезе сердце мое и плоть моя, Боже сердца моего, и часть моя, Боже, во век.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Яко се, удаляющии себе от Тебе погибнут: потребил еси всякаго любодеющаго от Тебе.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Мне же прилеплятися Богови благо есть, полагати на Господа упование мое, возвестити ми вся хвалы Твоя, во вратех дщере Сиони.

< Zaburi 73 >