< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Verdadeiramente bom é Deus para com Israel, para com os limpos de coração.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Emquanto a mim, os meus pés quasi que se desviaram; pouco faltou para que escorregassem os meus passos.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Pois eu tinha inveja dos loucos, quando via a prosperidade dos impios.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Porque não ha apertos na sua morte, mas firme está a sua força.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Não se acham em trabalhos como outra gente, nem são afflictos como outros homens.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Pelo que a soberba os cerca como um colar; vestem-se de violencia como de adorno.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Os olhos d'elles estão inchados de gordura: elles teem mais do que o coração podia desejar.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
São corrompidos e tratam maliciosamente de oppressão; fallam arrogantemente.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Põem as suas boccas contra os céus, e as suas linguas andam pela terra.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Pelo que o seu povo volta aqui, e aguas de copo cheio se lhes espremem.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
E dizem: Como o sabe Deus? ou ha conhecimento no Altissimo?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Eis que estes são impios, e prosperam no mundo; augmentam em riquezas.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Na verdade que em vão tenho purificado o meu coração; e lavei as minhas mãos na innocencia.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Pois todo o dia tenho sido afflicto, e castigado cada manhã.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Se eu dissesse: Fallarei assim; eis que offenderia a geração de teus filhos.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Quando pensava em entender isto foi para mim muito doloroso;
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Até que entrei no sanctuario de Deus: então entendi eu o fim d'elles.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Certamente tu os pozeste em logares escorregadios: tu os lanças em destruição.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Como caem na desolação, quasi n'um momento! ficam totalmente consumidos de terrores.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Como um sonho, quando se acorda, assim, ó Senhor, quando acordares, desprezarás a apparencia d'elles.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Assim o meu coração se azedou, e sinto picadas nos meus rins.
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Assim me embruteci, e nada sabia; fiquei como uma besta perante ti.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Todavia estou de continuo comtigo; tu me sustentaste pela minha mão direita.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Guiar-me-has com o teu conselho, e depois me receberás em gloria.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Quem tenho eu no céu senão a ti? e na terra não ha a quem eu deseje além de ti.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
A minha carne e o meu coração desfallecem; mas Deus é a fortaleza do meu coração, e a minha porção para sempre
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Pois eis que os que se alongam de ti, perecerão; tu tens destruido todos aquelles que se desviam de ti.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Mas para mim, bom é approximar-me de Deus; puz a minha confiança no Senhor Deus, para annunciar todas as tuas obras.

< Zaburi 73 >