< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Salmo di Asaf. Certo, Iddio è buono verso Israele, verso quelli che son puri di cuore.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Ma, quant’è a me, quasi inciamparono i miei piedi; poco mancò che i miei passi non sdrucciolassero.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Poiché io portavo invidia agli orgogliosi, vedendo la prosperità degli empi.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Poiché per loro non vi son dolori, il loro corpo è sano e pingue.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Non sono travagliati come gli altri mortali, né son colpiti come gli altri uomini.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Perciò la superbia li cinge a guisa di collana, la violenza li cuopre a guisa di vestito.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Dal loro cuore insensibile esce l’iniquità; le immaginazioni del cuor loro traboccano.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Sbeffeggiano e malvagiamente ragionan d’opprimere; parlano altezzosamente.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Metton la loro bocca nel cielo, e la loro lingua passeggia per la terra.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Perciò il popolo si volge dalla loro parte, e beve copiosamente alla loro sorgente,
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
e dice: Com’è possibile che Dio sappia ogni cosa, che vi sia conoscenza nell’Altissimo?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Ecco, costoro sono empi: eppure, tranquilli sempre, essi accrescono i loro averi.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Invano dunque ho purificato il mio cuore, e ho lavato le mie mani nell’innocenza!
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Poiché son percosso ogni giorno, e il mio castigo si rinnova ogni mattina.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Se avessi detto: Parlerò a quel modo, ecco, sarei stato infedele alla schiatta de’ tuoi figliuoli.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Ho voluto riflettere per intender questo, ma la cosa mi è parsa molto ardua,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
finché non sono entrato nel santuario di Dio, e non ho considerata la fine di costoro.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Certo, tu li metti in luoghi sdrucciolevoli, tu li fai cadere in rovina.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Come sono stati distrutti in un momento, portati via, consumati per casi spaventevoli!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Come avviene d’un sogno quand’uno si sveglia, così tu, o Signore, quando ti desterai, sprezzerai la loro vana apparenza.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Quando il mio cuore s’inacerbiva ed io mi sentivo trafitto internamente,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
ero insensato e senza conoscimento; io ero verso di te come una bestia.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Ma pure, io resto del continuo con te; tu m’hai preso per la man destra;
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
tu mi condurrai col tuo consiglio, e poi mi riceverai in gloria.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Chi ho io in cielo fuori di te? E sulla terra non desidero che te.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
La mia carne e il mio cuore posson venir meno, ma Dio è la ròcca del mio cuore e la mia parte in eterno.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Poiché, ecco, quelli che s’allontanan da te periranno; tu distruggi chiunque, fornicando, ti abbandona.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Ma quanto a me, il mio bene è d’accostarmi a Dio; io ho fatto del Signore, dell’Eterno, il mio rifugio, per raccontare, o Dio, tutte le opere tue.

< Zaburi 73 >