< Zaburi 73 >
1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Salmo di Asaf CERTAMENTE Iddio [è] buono ad Israele, A [quelli che son] puri di cuore.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Ora, quant'è a me, quasi che incapparono i miei piedi; Come nulla [mancò] che i miei passi non isdrucciolassero.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Perciocchè io portava invidia agl'insensati, Veggendo la prosperità degli empi.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Perciocchè non [vi sono] alcuni legami alla lor morte; E la lor forza [è] prosperosa.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
[Quando] gli [altri] uomini [sono] in travagli, essi non [vi son] punto; E non ricevono battiture col rimanente degli uomini.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Perciò, la superbia li cinge a giusa di collana; La violenza li involge [come] un vestimento.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Gli occhi escono loro fuori per lo grasso; Avanzano le immaginazioni del cuor [loro].
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Son dissoluti, e per malizia ragionano di oppressare; Parlano da alto.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Mettono la lor bocca dentro al cielo, E la lor lingua passeggia per la terra.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Perciò, il popolo di Dio riviene a questo, [Veggendo che] l'acqua gli è spremuta a bere a pien [calice],
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
E dice: Come [può essere che] Iddio sappia [ogni cosa], E che vi sia conoscimento nell'Altissimo?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Ecco, costoro [son] empi, e pur godono pace e tranquillità in perpetuo; Ed accrescono le [lor] facoltà.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Indarno [adunque] in vero ho nettato il mio cuore, Ed ho lavate le mie mani nell'innocenza.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Poichè son battuto tuttodì, Ed ogni mattina il mio gastigamento [si rinnuova].
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Se io dico: Io ragionerò così; Ecco, io son disleale inverso la generazione de' tuoi figliuoli.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Io ho adunque pensato di [volere] intender questo; Ma [la cosa] mi è parsa molto molesta.
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Infino a tanto che sono entrato ne' santuari di Dio; [Ed] ho considerato il fine di coloro.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Certo, tu li metti in isdruccioli; Tu li trabocchi in ruine.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Come sono eglino stati distrutti in un momento! [Come] son venuti meno, e sono stati consumati per casi spaventevoli!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
[Son] come un sogno, dopo che [l'uomo] si è destato; O Signore, quando tu [ti] risveglierai, tu sprezzerai la lor vana apparenza.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Quando il mio cuore era inacerbito, Ed io era punto nelle reni;
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Io [era] insensato, e non aveva conoscimento; Io era inverso te [simile] alle bestie.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Ma pure io sono stato del continuo teco; Tu mi hai preso per la man destra.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Tu mi condurrai per lo tuo consiglio, E poi mi riceverai [in] gloria;
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Chi [è] per me in cielo, [fuor che te?] Io non voglio [altri] che te in terra.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
La mia carne ed il mio cuore erano venuti meno: [Ma] Iddio [è] la rocca del mio cuore, e la mia parte in eterno.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Perciocchè, ecco, quelli che si allontanano da te periranno; Tu distruggerai ogni uomo che fornica[ndo si svia] da te.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Ma quant'è a me, egli mi [è] buono di accostarmi a Dio; Io ho posta nel Signore Iddio la mia confidanza, Per raccontar tutte le opere sue.