< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
מזמור לאסף אך טוב לישראל אלהים-- לברי לבב
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
ואני--כמעט נטוי (נטיו) רגלי כאין שפכה (שפכו) אשרי
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
כי-קנאתי בהוללים שלום רשעים אראה
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
כי אין חרצבות למותם ובריא אולם
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
בעמל אנוש אינמו ועם-אדם לא ינגעו
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
לכן ענקתמו גאוה יעטף-שית חמס למו
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
יצא מחלב עינמו עברו משכיות לבב
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
ימיקו וידברו ברע עשק ממרום ידברו
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
שתו בשמים פיהם ולשונם תהלך בארץ
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
לכן ישיב (ישוב) עמו הלם ומי מלא ימצו למו
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
ואמרו איכה ידע-אל ויש דעה בעליון
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
הנה-אלה רשעים ושלוי עולם השגו-חיל
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
אך-ריק זכיתי לבבי וארחץ בנקיון כפי
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
ואהי נגוע כל-היום ותוכחתי לבקרים
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
אם-אמרתי אספרה כמו הנה דור בניך בגדתי
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
ואחשבה לדעת זאת עמל היא (הוא) בעיני
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
עד-אבוא אל-מקדשי-אל אבינה לאחריתם
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
אך בחלקות תשית למו הפלתם למשואות
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
איך היו לשמה כרגע ספו תמו מן-בלהות
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
כחלום מהקיץ-- אדני בעיר צלמם תבזה
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
כי יתחמץ לבבי וכליותי אשתונן
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
ואני-בער ולא אדע בהמות הייתי עמך
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
ואני תמיד עמך אחזת ביד-ימיני
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
בעצתך תנחני ואחר כבוד תקחני
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
מי-לי בשמים ועמך לא-חפצתי בארץ
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
כלה שארי ולבבי צור-לבבי וחלקי--אלהים לעולם
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
כי-הנה רחקיך יאבדו הצמתה כל-זונה ממך
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
ואני קרבת אלהים-- לי-טוב שתי באדני יהוה מחסי לספר כל-מלאכותיך

< Zaburi 73 >