< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Ein Psalm Asaphs. Nur gut ist Gott gegen Israel, gegen die, welche reinen Herzens sind.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Ich aber hätte schier gestrauchelt mit meinen Füßen, wie leicht hätte ich einen Mißtritt getan!
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Denn ich beneidete die Übermütigen, als ich den Frieden der Gottlosen sah.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Denn sie leiden keine Qual bis zu ihrem Tod, und ihr Leib ist wohlgenährt.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Sie werden nicht bemüht wie andere Leute und nicht geschlagen wie andere Menschen.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Darum schmücken sie sich stolz und kleiden sich frech.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Ihr Gesicht strotzt von Fett, sie bilden sich sehr viel ein.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Sie reden höhnisch und boshaft, drohen mit höherer Gewalt.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Sie reden, als käme es vom Himmel; ihre Worte haben Geltung auf Erden.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Darum wendet sich auch das Volk ihnen zu, und es wird von ihnen viel Wasser aufgesogen.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Und sie sagen: «Was merkt Gott? Weiß der Höchste überhaupt etwas?»
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Siehe, das sind die Gottlosen; denen geht es immer gut, und sie werden reich!
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Ganz umsonst habe ich mein Herz rein erhalten und meine Hände in Unschuld gewaschen;
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
denn ich bin doch täglich geschlagen worden, und meine Strafe ist alle Morgen da!
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Wollte ich auch so rechnen, siehe, so würde ich das Geschlecht deiner Kinder verraten.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
So sann ich denn nach, um dies zu verstehen; aber es schien mir vergebliche Mühe zu sein,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
bis ich in das Heiligtum Gottes ging und auf ihr Ende merkte.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Nur auf schlüpfrigen Boden setzest du sie; du lässest sie fallen, daß sie in Trümmer sinken.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Wie geschah das so plötzlich und entsetzlich! Sie gingen unter und nahmen ein Ende mit Schrecken.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Wie einen Traum nach dem Erwachen, so wirst du, o Herr, wenn du dich aufmachst, ihr Bild verächtlich machen.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Als mein Herz verbittert war und es mir in den Nieren wehe tat,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
da war ich dumm und verstand nichts; ich benahm mich wie ein Vieh gegen dich.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Und doch bleibe ich stets bei dir; du hältst mich bei meiner rechten Hand.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Leite mich auch ferner nach deinem Rat und nimm mich hernach mit Ehren auf!
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Wen habe ich im Himmel? Und dir ziehe ich gar nichts auf Erden vor!
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Schwinden auch mein Fleisch und mein Herz dahin, so bleibt doch Gott ewiglich meines Herzens Fels und mein Teil.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Denn siehe, die fern von dir sind, kommen um; du vertilgst alle, die dir untreu werden.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Mir aber ist die Nähe Gottes köstlich; ich habe Gott, den HERRN, zu meiner Zuflucht gemacht, um zu erzählen alle deine Werke.

< Zaburi 73 >