< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Ein Psalm Asaphs. Ja, gütig ist Gott gegen Israel, gegen die, die reines Herzens sind.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Meine Füße aber hätten beinahe gestrauchelt; nichts fehlte, so wären meine Tritte ausgeglitten.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Denn ich ereiferte mich wegen der Übermütigen, wenn ich sah, daß es den Gottlosen so wohl ging.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Denn sie leiden keine Schmerzen, kräftig und wohlgenährt ist ihr Leib.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Sie geraten nicht in Unglück, wie andere Leute, und werden nicht wie andere Menschen geplagt.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Darum ist Hochmut ihr Halsgeschmeide, Gewaltthat umhüllt sie als Gewand.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Aus der Verfettung stammt ihre Verschuldung, wallen die Gebilde ihres Herzens über.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Sie höhnen und reden in Bosheit, reden Bedrückung von oben herab.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
In den Himmel erheben sie ihr Maul, während sich ihre Zunge auf Erden ergeht.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Darum wendet sich sein Volk hierher, und Wasser in Fülle wird von ihnen geschlürft.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Sie sprechen: “Wie weiß es Gott, und wie gäbe es ein Wissen darum beim Höchsten?”
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Ja, so sind die Gottlosen und in steter Ruhe häufen sie Reichtum an.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
War es denn ganz umsonst, daß ich mein Herz rein erhielt und in Unschuld meine Hände wusch -
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
und ward doch immerfort geplagt, und alle Morgen war meine Züchtigung da?
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Wenn ich dächte: Solches will ich verkündigen, so hätte ich das Geschlecht deiner Kinder verleugnet!
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Da sann ich nach, um es zu begreifen, aber ein Elend war es in meinen Augen,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
bis ich in Gottes Heiligtümer eindrang, acht hatte auf ihr Ende.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Ja, auf schlüpfrigen Boden stellst du sie, stürzest sie in Trümmer.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Wie sind sie im Nu zur Wüste geworden, haben ein Ende genommen, sind durch Schrecknisse dahin!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Gleich einem Traume nach dem Erwachen, so verschmähst du, Herr, wenn du wach wirst, ihr Bild.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Als mein Herz verbittert war, und es mich in den Nieren stach,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
da war ich unvernünftig und wußte nichts, war dir gegenüber wie ein Vieh.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Aber ich bleibe stets bei dir; du hältst mich bei meiner rechten Hand.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Nach deinem Ratschlusse wirst du mich leiten und mich darnach zu Ehren annehmen.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Wen habe ich im Himmel? und außer dir begehre ich nichts auf Erden.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Wäre gleich mein Fleisch und mein Herz dahingeschwunden - Gott ist immerdar meines Herzens Fels und mein Teil!
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Denn fürwahr, die sich von dir fern halten, kommen um; du vertilgst einen jeden, der dir treulos wird.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Mir aber ist die Nähe Gottes köstlich; in den Herrn Jahwe habe ich meine Zuflucht gesetzt, um von allen deinen Werken zu erzählen.

< Zaburi 73 >