< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Ein Lied, von Asaph. - Gewiß! Das höchste Gut für Israel ist Gott, für die, die reinen Herzens sind.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Ich wäre fast mit meinem Fuß gestrauchelt; fast hätte einen Fehltritt ich getan.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Denn ich beneidete die Übermütigen und gaffte bei der Frevler Wohlergehen.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Denn ihre Sklaven brauchen keine Fesseln, und kerngesund ist ihr Gesinde.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Sie teilen nicht der Menschen Leid und werden nicht wie andere geplagt.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Drum ist ihr Halsgeschmeide Übermut; Gewalttat heißt das Kleid, das sie umhüllt.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Ihr Auge quillt aus Fett hervor; ausschweifend sind des Herzens Süchte.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Sie reden boshaft, voller Hohn, und drohen mit Gewalt von oben her.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Mit ihrem Munde tasten sie den Himmel an, und ihre Zunge herrscht durchs ganze Land-
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
"Fürwahr! Dahin hat er sein Volk gebracht, daß sie nicht Wasser zur Genüge fanden."
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Sie sprechen: "Ach, wie weiß denn Gott? Gibt's denn ein Wissen bei dem Höchsten?"
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Ja, diese sind so frevelhaft und glücklich in der Welt, vermehren sie ihr Hab und Gut.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
So hielt ich denn vergeblich rein mein Herz und wusch in Unschuld meine Hände?
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Den ganzen Tag bin ich geplagt, und meine Züchtigung ist jeden Morgen da.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Nähm ich mir aber vor, also zu sprechen: "So geht es dem Geschlechte Deiner Kinder", so wär's von mir vermessen.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Wenn ich's nachsinnend will verstehen, da wird's in meinen Augen erst ein Jammer,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
bis ich in Gottes heilige Pläne dringe. Da erst begreife ich ihr Ziel:
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Du stellst sie auf gar schlüpferigen Boden, daß Du sie ins Verderben stürzest.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Wie plötzlich gehen sie zugrunde! Wie schrecklich werden sie dahingerafft, vertilgt!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Wie beim Erwachen einen Traum der Wachende verachtet, so tust Du's, Herr, mit ihrem Schatten.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Wenn voll von Bitternis das Herz mir wäre, und schnitte durch die Nieren mir der Schmerz,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
dann wäre ich ein Tier, ganz unverständig, ein unvernünftig Tier vor Dir.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Doch immer bleibe ich Dir treu, wenn Du mich bei der Rechten fassest
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
und leitest mich nach Deinem Rat und nimmst zuletzt mich noch zu Besserm mit.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Wen habe ich im Himmel? Und wenn ich Dich besitze, brauche ich auf dieser Welt nichts mehr.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Vergeht mein Fleisch, mein Herz, so bleibt doch meines Herzens Hort, mein Anteil Gott in Ewigkeit.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Wer sich von Dir entfernt, kommt um. Jedweden tilgst Du, der Dir Treue kündigt.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Für mich ist's Seligkeit, mich Gott zu nahen. Ich setze meine Hoffnung auf den Herrn, den Herrn, daß ich verkünden kann, was immer Du verheißen hast.

< Zaburi 73 >