< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Psaume d'Asaph. Oui, Dieu est bon pour Israël, Pour ceux qui ont le coeur pur.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Cependant, mes pieds ont failli broncher: Il s'en est fallu de peu que j'aie glissé!
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
En effet, j'ai porté envie aux orgueilleux, Quand j'ai vu la prospérité des méchants!
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Car ils sont exempts de souffrance; Leur corps demeure vigoureux et robuste.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Ils n'ont aucune part aux peines des mortels; Ils ne sont point frappés avec les autres humains.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
C'est pourquoi, ils se parent d'orgueil comme d'un collier; La violence les couvre comme un vêtement.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Ils sont bouffis de graisse, pleins d'iniquité, Et leur coeur déborde de mauvaises pensées.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Ils ricanent, ils se vantent méchamment de leurs violences; Leurs paroles sont hautaines.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Leur bouche s'élève contre le ciel, Et leur langue sème la calomnie sur la terre.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Aussi attirent-ils à leur cause une foule de gens Qui boivent avidement leurs paroles,
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Et qui disent: «Comment le Dieu fort pourrait-il savoir? Comment le Très-Haut connaîtrait-il?»
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Tels sont les méchants: Toujours heureux, ils amassent des richesses.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
C'est donc en vain que j'ai gardé mon coeur pur, Et que j'ai lavé mes mains dans l'innocence;
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Car je suis frappé tous les jours, Et le châtiment tombe chaque matin sur moi.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Si j'avais dit: «Je parlerai comme eux» — Alors, j'aurais été infidèle à la race de tes enfants.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
J'ai donc cherché à comprendre ces choses; Mais la tâche a été trop pénible pour moi,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Jusqu'au moment où je suis entré Dans les sanctuaires du Dieu fort, Et où j'ai fait attention à la fin de ces gens-là.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Oui, tu les mets sur un terrain glissant; Tu les fais tomber, et ils s'écroulent!
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Comme ils sont détruits en un moment. Enlevés et consumés par une destruction soudaine!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Tel un songe, quand on s'éveille. Ainsi, Seigneur, quand tu te lèves, Tu les dissipes comme de vains fantômes.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Quand l'amertume remplissait mon coeur, Et que je me tourmentais en moi-même,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Alors j'étais sans raison et sans intelligence; J'étais à tes yeux comme un animal stupide.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Cependant, je resterai toujours avec toi: Tu m'as pris par la main droite.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Tu me guideras par ta sagesse. Et puis, tu m'introduiras dans la gloire.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Quel autre que toi ai-je au ciel? Sur la terre aussi, je ne prends plaisir qu'en toi.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Quand même ma chair et mon coeur seraient consumés, Dieu est le rocher de mon coeur, et mon partage pour toujours.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Oui, ceux qui s'éloignent de toi périront; Tu détruis tous ceux qui se détournent de toi.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Pour moi, m'approcher de Dieu, c'est mon bonheur; Je mets ma confiance dans le Seigneur, l'Éternel, Afin de raconter toutes ses oeuvres.

< Zaburi 73 >