< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Cantique d'Asaph. Oui, Dieu est bon envers Israël, envers ceux qui ont un cœur pur.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Cependant mon pied fut bien près de broncher; un rien eût déroulé mes pas;
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
car j'enviais les superbes: j'avais le bonheur des impies sous les yeux.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Car ils sont exempts de douleurs jusqu'à leur mort, et leur corps est bien entretenu;
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
ils sont en dehors des peines des mortels, et comme les humains ils ne sont point frappés.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Aussi, comme un collier l'orgueil les entoure, et comme un habit la violence les revêt.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
L'embonpoint rend leurs yeux saillants, et les pensées de leur cœur se produisent.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Ils sont moqueurs, et parlent méchamment; de leur hauteur ils parlent d'opprimer;
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
de leur bouche ils affrontent le ciel même, et leur langue se démène sur la terre.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Aussi, c'est de ce côté que Son peuple se tourne; il veut aussi s'abreuver aux eaux abondantes,
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
et dit: « Comment Dieu prendrait-il connaissance, et le Tout-puissant aurait-Il la science? »
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Les voilà ces impies! et toujours tranquilles ils grossissent leurs trésors.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
C'est en pure perte que je gardai mon cœur net, et que je lavai mes mains dans l'innocence;
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
et je fus frappé tous les jours, et chaque matin je subis ma peine.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Si je disais: Je veux parler ainsi, voici, je trahirais la race de tes enfants.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Alors je réfléchis, pour me rendre compte de ces choses; c'était à mes yeux une tâche difficile,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
jusqu'à ce que, pénétrant dans les sanctuaires de Dieu, je fis attention à la fin de ces hommes
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Tu ne les as placés que sur un sol glissant; tu les fait tomber, et ils sont en ruine.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Comme ils sont anéantis tout à coup, emportés et détruits par une chute soudaine!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Tel un songe au réveil, ainsi, les réveillant, Seigneur, tu mets avec mépris leur fantôme à néant.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Quand mon cœur s'exaspérait, et que dans mes reins je sentais l'aiguillon,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
alors j'étais stupide, et dans l'ignorance, j'étais disposé comme une brute envers toi.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Cependant je te demeurai toujours attaché; tu me pris par la main, par ma droite.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Par ta sagesse tu me conduiras, et enfin tu me recueilleras dans la gloire.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Qui ai-je dans les Cieux? Et auprès de toi je n'aime rien sur la terre.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Que mon cœur et ma chair soient consumés, le rocher de mon cœur et ma part, c'est Dieu, à jamais!
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Car voici, ceux qui te désertent, périssent; tu détruis tous ceux qui loin de toi vont se prostituer.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Mais pour moi, être près de Dieu, c'est mon bien. Je mets ma confiance dans le Seigneur, l'Éternel, afin de pouvoir raconter toutes tes œuvres.

< Zaburi 73 >