< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Psaume d'Asaph. Oui, Dieu est bon pour Israël, pour ceux qui ont le cœur pur.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Pour moi, le pied m'a presque manqué, et peu s'en est fallu que mes pas n'aient glissé;
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Car j'ai porté envie aux insensés, voyant la prospérité des méchants.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Car ils ne sont point liés jusqu'à leur mort, et leur force est en son entier.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Quand les mortels sont en peine, ils n'y sont point; ils ne sont point frappés avec les humains.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
C'est pourquoi l'orgueil les entoure comme un collier, la violence les couvre comme un vêtement.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Leurs yeux sont enflés à force d'embonpoint; les désirs de leur cœur se font jour.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Ils sont moqueurs et parlent méchamment d'opprimer; ils parlent avec hauteur.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Ils portent leur bouche jusqu'au ciel, et leur langue parcourt la terre.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Aussi son peuple en revient à ceci, quand on leur fait boire les eaux amères en abondance,
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Et ils disent: Comment Dieu connaîtrait-il? Et comment y aurait-il de la connaissance chez le Très-Haut?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Voici, ceux-là sont des méchants, et, toujours heureux, ils amassent des richesses.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Certainement c'est en vain que j'ai purifié mon cœur, et que j'ai lavé mes mains dans l'innocence.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Car je suis frappé tous les jours, et mon châtiment revient chaque matin.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Si j'ai dit: Je parlerai ainsi; voici, j'étais infidèle à la race de tes enfants.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
J'ai donc réfléchi pour comprendre ces choses, et cela m'a semblé fort difficile;
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Jusqu'à ce qu'entré dans les sanctuaires de Dieu, j'aie pris garde à la fin de ces gens-là.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Car tu les mets en des lieux glissants; tu les fais tomber dans des précipices.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Comme ils sont détruits en un moment! enlevés et consumés par une destruction soudaine!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Tel un songe quand on s'éveille, ainsi, Seigneur, à ton réveil tu mets en mépris leur vaine apparence.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Quand mon cœur s'aigrissait ainsi, et que je me tourmentais en moi-même,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Alors j'étais abruti et sans connaissance; j'étais devant toi comme les bêtes.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Mais moi, je serai toujours avec toi; tu m'as pris par la main droite.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Tu me conduiras par ton conseil, puis tu me recevras dans la gloire.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Quel autre que toi ai-je au ciel? Je ne prends plaisir sur la terre qu'en toi.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Ma chair et mon cœur défaillaient; mais Dieu est le rocher de mon cœur et mon partage à toujours.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Car voici: ceux qui s'éloignent de toi périront. Tu retranches tous ceux qui se détournent de toi.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Mais pour moi, m'approcher de Dieu, c'est mon bien; j'ai placé mon refuge dans le Seigneur, l'Éternel, afin de raconter toutes tes œuvres.

< Zaburi 73 >