< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Psaume d'Asaph. Quoi qu'il en soit, Dieu est bon à Israël, [savoir], à ceux qui sont nets de cœurs.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
Or quant à moi, mes pieds m'ont presque manqué, [et] il s'en est peu fallu que mes pas n'aient glissé.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Car j'ai porté envie aux insensés, en voyant la prospérité des méchants.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Parce qu'il n'y a point d'angoisses en leur mort, mais leur force est en son entier.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Ils ne sont point en travail avec les [autres] hommes, et ils ne sont point battus avec les [autres] hommes.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
C'est pourquoi l'orgueil les environne comme un collier, et un vêtement de violence les couvre.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Les yeux leur sortent dehors à force de graisse; ils surpassent les desseins de [leur] cœur.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Ils sont pernicieux, et parlent malicieusement d'opprimer; ils parlent comme placés sur un lieu élevé.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Ils mettent leur bouche aux cieux, et leur langue parcourt la terre.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
C'est pourquoi son peuple en revient là, quand on lui fait sucer l'eau à plein [verre].
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
Et ils disent: comment le [Dieu] Fort connaîtrait-il, et y aurait-il de la connaissance au Souverain?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Voilà, ceux-ci sont méchants, et étant à leur aise en ce monde, ils acquièrent de plus en plus des richesses.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Quoi qu'il en soit, c'est en vain que j'ai purifié mon cœur, et que j'ai lavé mes mains dans l'innocence.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
Car j'ai été battu tous les jours, et mon châtiment revenait tous les matins.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
[Mais] quand j'ai dit: j'en parlerai ainsi; voilà, j'ai été infidèle à la génération de tes enfants.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Toutefois j'ai tâché à connaître cela; mais cela m'a paru fort difficile.
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Jusques à ce que je sois entré au sanctuaire du [Dieu] Fort, [et] que j'aie considéré la fin de telles gens.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Quoi qu'il en soit, tu les as mis en des lieux glissants, tu les fais tomber dans des précipices.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Comment ont-ils été ainsi détruits en un moment? sont-ils défaillis? ont-ils été consumés d'épouvantements?
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Ils sont comme un songe lorsqu'on s'est réveillé. Seigneur tu mettras en mépris leur ressemblance quand tu te réveilleras.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
[Or] quand mon cœur s'aigrissait, et que je me tourmentais en mes reins;
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
J'étais alors stupide, et je n'avais aucune connaissance; j'étais comme une brute en ta présence.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Je serai donc toujours avec toi; tu m'as pris par la main droite,
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Tu me conduiras par ton conseil, et puis tu me recevras dans la gloire.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Quel autre ai-je au Ciel? Or je n'ai pris plaisir sur la terre en rien qu'en toi seul.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Ma chair et mon cœur étaient consumés; mais Dieu est le rocher de mon cœur, et mon partage à toujours.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Car voilà, ceux qui s'éloignent de toi, périront; tu retrancheras tous ceux qui se détournent de toi.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Mais pour moi, approcher de Dieu est mon bien; j'ai mis toute mon espérance au Seigneur Eternel, afin que je raconte tous tes ouvrages.

< Zaburi 73 >