< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
A Psalm of Asaph. Truly God is good to Israel, even to such as are of a clean heart.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
But as for me, my feet were almost gone; my steps had almost slipped.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
For I was envious at the foolish, when I saw the prosperity of the wicked.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
For there are no pangs in their death: but their strength is firm.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
They are not in trouble as other men; neither are they afflicted like other men.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Therefore pride surroundeth them as a chain; violence covereth them as a garment.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Their eyes stand out with fatness: they have more than heart could wish.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
They are corrupt, and speak wickedly concerning oppression: they speak loftily.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
They set their mouth against the heavens, and their tongue walketh through the earth.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Therefore his people return here: and waters of a full cup are wrung out to them.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
And they say, How doth God know? and is there knowledge in the most High?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Behold, these are the ungodly, who prosper in the world; they increase in riches.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Verily I have cleansed my heart in vain, and washed my hands in innocency.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
For all the day long have I been afflicted, and chastened every morning.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
If I say, I will speak thus; behold, I should offend against the generation of thy children.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
When I thought to know this, it was too painful for me;
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Until I went into the sanctuary of God; then I understood their end.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Surely thou didst set them in slippery places: thou didst cast them down into destruction.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
How are they brought into desolation, as in a moment! they are utterly consumed with terrors.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
As a dream when one awaketh; so, O Lord, when thou awakest, thou shalt despise their image.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Thus my heart was grieved, and I was pricked in my reins.
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
So foolish was I, and ignorant: I was as a beast before thee.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Nevertheless I am continually with thee: thou hast held me by my right hand.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Thou shalt guide me with thy counsel, and afterward receive me to glory.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Whom have I in heaven but thee? and there is none upon earth that I desire besides thee.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
My flesh and my heart faileth: but God is the strength of my heart, and my portion for ever.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For, lo, they that are far from thee shall perish: thou hast destroyed all them that go astray from thee.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
But it is good for me to draw near to God: I have put my trust in the Lord GOD, that I may declare all thy works.

< Zaburi 73 >