< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
A psalm of Asaph. Yes, God is good to the upright, the Lord to the pure in heart.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
But my feet were almost gone, my steps had nearly slipped,
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
through envy of godless braggarts, when I saw how well they fared.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
For never a pang have they, their body is sound and sleek.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
They have no trouble like mortals, no share in human pain.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
So they wear their pride like a necklace, they put on the garment of wrong,
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
their eyes stand out with fatness, their heart swells with riotous fancies.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Their speech is mocking and evil, condescending and crooked their speech.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
They have set their mouth in the heavens, while their tongue struts about on the earth.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Small wonder that people resort to them, and drink deep draughts of their lore.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
‘How does God know?’ they say, ‘And has the Most High any knowledge?’
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
See! These are the godless, with wealth and ease ever increasing.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Yes, in vain have I kept my heart pure, and washed my hands in innocence;
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
for all the day long was I plagued not a morning but I was chastised.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
But to resolve to speak like they do would be treachery to your children.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
So I sought to understand it, but a wearisome task it seemed:
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
till I entered the holy world of God and saw clearly their destiny.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Yes, you set them on slippery places; down to destruction you hurl them.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
One moment and then what a horror of ruin! They are finished and ended in terrors.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Like a dream, when one wakes, shall they be, whose phantoms the waker despises.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
So my bitterness of mind and the pain that stabbed my heart
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
show how dull I was and stupid just like a beast before you.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
But I am always with you, you have hold of my right hand.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
By a plan of yours you guide me and will afterward take me to glory.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Whom have I in the heavens but you? And on earth there is none I desire beside you.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Though flesh and heart waste away, yet God is the rock of my heart, yet God is my portion forever.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For see! Those who are far from you must perish, you destroy all who are false to you.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
But I am happy when close to God; the Lord my God I have made my refuge, that I may recount all the things you have done.

< Zaburi 73 >