< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
[A Psalm by Asaph.] Surely God is good to Israel, to those who are pure in heart.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
But as for me, my feet were almost gone. My steps had nearly slipped.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
For I was envious of the arrogant, when I saw the prosperity of the wicked.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
For there are no struggles in their death, but their strength is firm.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
They are free from burdens of men, neither are they plagued like other men.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Therefore pride is like a chain around their neck. Violence covers them like a garment.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Their sin proceeds forth from fatness. Their hearts overflow with imaginations.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
They scoff and speak with malice. In arrogance, they threaten oppression.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
They have set their mouth in the heavens. Their tongue walks through the earth.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Therefore his people turn to them, and they drink up waters of abundance.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
They say, "How does God know? Is there knowledge in the Most High?"
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Look, these are the wicked. Being always at ease, they increase in riches.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Surely in vain I have cleansed my heart, and washed my hands in innocence,
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
For all day long have I been plagued, and punished every morning.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
If I had said, "I will speak thus;" look, I would have betrayed the generation of your children.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
When I tried to understand this, it was too painful for me;
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Until I entered God's sanctuary, and considered their latter end.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Surely you set them in slippery places. You throw them down to destruction.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
How they are suddenly destroyed. They are completely swept away with terrors.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
As a dream when one wakes up, so, LORD, when you awake, you will despise their fantasies.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
For my soul was grieved. I was embittered in my heart.
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
I was so senseless and ignorant. I was a brute beast before you.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Nevertheless, I am continually with you. You have held my right hand.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
You will guide me with your counsel, and afterward receive me to glory.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Who do I have in heaven? There is no one on earth who I desire besides you.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
My flesh and my heart fails, but God is the strength of my heart and my portion forever.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For, look, those who are far from you shall perish. You have destroyed all those who are unfaithful to you.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
But it is good for me to come close to God. I have made the LORD my refuge, that I may tell of all your works in the gates of the daughter of Zion.

< Zaburi 73 >