< Zaburi 73 >
1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
A Psalm of Asaph. Truly God is good to Israel, to such as are of a pure heart.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
But as for me, my feet were almost gone, my steps had well nigh slipped;
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
For I was envious at the arrogant, seeing the prosperity of the wicked.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
For they have no pangs in their death, and their body is well nourished;
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
They have not the hardships of mankind, neither are they plagued like [other] men:
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Therefore pride encompasseth them as a neck-chain, violence covereth them [as] a garment;
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Their eyes stand out from fatness, they exceed the imaginations of their heart:
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
They mock and speak wickedly of oppression, they speak loftily:
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
They set their mouth in the heavens, and their tongue walketh through the earth.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Therefore his people turn hither, and waters in fulness are wrung out to them.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
And they say, How can God know, and is there knowledge in the Most High?
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Behold, these are the wicked, and they prosper in the world: they heap up riches.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Truly have I purified my heart in vain, and washed my hands in innocency:
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
For all the day have I been plagued, and chastened every morning.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
If I said, I will speak thus, behold, I should be faithless to the generation of thy children.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
When I thought to be able to know this, it was a grievous task in mine eyes;
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
Until I went into the sanctuaries of God; [then] understood I their end.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Truly thou settest them in slippery places, thou castest them down in ruins.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
How are they suddenly made desolate! they pass away, consumed with terrors.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
As a dream, when one awaketh, wilt thou, Lord, on arising despise their image.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
When my heart was in a ferment, and I was pricked in my reins,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Then I was brutish and knew nothing; I was [as] a beast with thee.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Nevertheless I am continually with thee: thou hast holden my right hand;
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Thou wilt guide me by thy counsel, and after the glory, thou wilt receive me.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Whom have I in the heavens? and there is none upon earth I desire beside thee.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
My flesh and my heart faileth: God is the rock of my heart and my portion for ever.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For behold, they that are far from thee shall perish; thou destroyest every one that goeth a whoring from thee.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
But as for me, it is good for me to draw near to God: I have put my trust in the Lord Jehovah, that I may declare all thy works.