< Zaburi 73 >
1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
A Psalm of Asaph. How good is God to Israel, to those who are upright in heart.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
But my feet were nearly moved; my steps had nearly slipped.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
For I was zealous over the iniquitous, seeing the peacefulness of sinners.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
For they have no respect for their death, nor do they have support in their wounds.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
They are not with the hardships of men, nor will they be scourged with men.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Therefore, arrogance has held on to them. They have been covered with their iniquity and impiety.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Their iniquity has proceeded, as if from fat. They have parted from the affection of the heart.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
They have thought and spoken wickedness. They have spoken iniquity in high places.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
They have set their mouth against heaven, and their tongue has traversed the earth.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Therefore, my people will be converted here, and fullness of days will be found in them.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
And they said, “How would God know?” and, “Isn’t there knowledge in high places?”
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Behold, these are sinners, and, abounding in this age, they have obtained riches.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
And I said: So then, it is without purpose that I have justified my heart and washed my hands among the innocent.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
And I have been scourged all day long, and I have received my chastisement in the mornings.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
If I were to say that I would explain this: Behold, I would condemn this nation of your sons.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
I considered, so that I might know this. It is a hardship before me,
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
until I may enter into the Sanctuary of God, and understand it to its last part.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
So, because of deceitfulness, truly, you have placed it before them. While they were being lifted up, you were casting them down.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
How have they been brought to desolation? They have suddenly failed. They have perished because of their iniquity.
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
As a dream is to those who awaken, O Lord, so will you reduce their image to nothing in your city.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
For my heart has been inflamed, and my temperament has been changed.
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
And so, I have been reduced to nothing, and I did not know it.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
I have become like a beast of burden to you, and I am always with you.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
You have held my right hand. And in your will, you have conducted me, and with your glory, you have taken me up.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
For what is there for me in heaven? And what do I wish for on earth before you?
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
My body has failed, and my heart: O God of my heart, and God my portion, into eternity.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
For behold, those who put themselves far from you will perish. You have perished all those who fornicate away from you.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
But it is good for me to adhere to God, to put my hope in the Lord God, so that I may announce all your prophecies, at the gates of the daughter of Zion.