< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
A Psalm of Asaph. Surely God is good to Israel, to those who are pure in heart.
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
But as for me, my feet had almost stumbled; my steps had nearly slipped.
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
For I envied the arrogant when I saw the prosperity of the wicked.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
They have no struggle in their death; their bodies are well-fed.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
They are free of the burdens others carry; they are not afflicted like other men.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Therefore pride is their necklace; a garment of violence covers them.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
From their prosperity proceeds iniquity; the imaginations of their hearts run wild.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
They mock and speak with malice; with arrogance they threaten oppression.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
They set their mouths against the heavens, and their tongues strut across the earth.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
So their people return to this place and drink up waters in abundance.
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
The wicked say, “How can God know? Does the Most High have knowledge?”
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Behold, these are the wicked— always carefree as they increase their wealth.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Surely in vain I have kept my heart pure; in innocence I have washed my hands.
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
For I am afflicted all day long and punished every morning.
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
If I had said, “I will speak this way,” then I would have betrayed Your children.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
When I tried to understand all this, it was troublesome in my sight
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
until I entered God’s sanctuary; then I discerned their end.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Surely You set them on slick ground; You cast them down into ruin.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
How suddenly they are laid waste, completely swept away by terrors!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Like one waking from a dream, so You, O Lord, awaken and despise their form.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
When my heart was grieved and I was pierced within,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
I was senseless and ignorant; I was a brute beast before You.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Yet I am always with You; You hold my right hand.
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
You guide me with Your counsel, and later receive me in glory.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Whom have I in heaven but You? And on earth I desire no one besides You.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
My flesh and my heart may fail, but God is the strength of my heart and my portion forever.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Those far from You will surely perish; You destroy all who are unfaithful to You.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
But as for me, it is good to draw near to God. I have made the Lord GOD my refuge, that I may proclaim all Your works.

< Zaburi 73 >