< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
Psalam. Asafov Kako je dobar Bog čestitima, Bog onima koji su čista srca!
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
A meni umalo noge ne posrnuše, zamalo koraci ne okliznuše,
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
jer zločincima zavidjeh motreći sreću grešnika.
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
Nikakvu patnju ne snose, pretilo je tijelo njihovo.
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
Ne žive u mukama smrtnika, ljudske ih nevolje ne biju.
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
Stoga je oholost ogrlica vratu njihovu, a nasilje haljina koja ih pokriva.
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
Iz pretila srca izlazi opakost njihova, srca im se prelijevaju ispraznim tlapnjama.
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
Podsmjehuju se i zlobno govore, nasiljem prijete odozgo.
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
Ustima na nebo nasrću, a jezik se njihov obara na zemlju.
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
Zato moj narod za njima leti i srče obilne vode
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
pa veli: “Kako da dozna Bog? Spoznaje li Svevišnji?”
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Eto, takvi su grešnici: uvijek spokojni, bogatstvo zgrću.
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
Jesam li, dakle, samo ja uzalud čuvao srce čisto i u nedužnosti prao ruke
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
kad sam primao udarce svaki dan i kaznu jutro za jutrom?
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
Da sam kazao: “Govorit ću kao i oni”, izdao bih rod sinova tvojih.
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Promišljah tada da bih spoznao: al' mi se učini mučno u očima mojim
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
sve dok ne nađoh ulaz u Božje svetinje pa prozreh kakav im je svršetak.
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
Zaista, na klizavu stazu ti ih postavljaš, u propast ih obaraš.
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
Kako učas propadoše, nestaše, užas ih izjede!
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Kao što čovjek prezire san kad se probudi, tako ćeš, Gospode, prezreti lik im kada ustaneš.
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
Kad mi duša bijaše ojađena, a bubrezi probodeni,
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
bezumnik bijah bez razbora, k'o živinče pred tobom.
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Al' ću odsad uvijek biti s tobom, jer ti prihvati desnicu moju:
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
vodit ćeš me po naumu svojem da me zatim uzmeš u slavu svoju.
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Koga ja imam u nebu osim tebe? Kad sam s tobom, ne veselim se zemlji.
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Malaksalo mi tijelo i srce: okrilje srca moga, i baštino moja, o Bože, dovijeka!
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Doista, propast će oni koji se udaljuju od tebe, istrebljuješ svakog tko ti se iznevjeri.
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
A meni je milina biti u Božjoj blizini, imati sklonište svoje u Jahvi. Pripovijedat ću sva tvoja djela na vratima Kćeri sionske.

< Zaburi 73 >