< Zaburi 73 >

1 Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
阿撒夫的詩歌。
2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
天主待正直的人多麼美善,上主對心裏潔淨的人亦然!
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
我的腳幾乎要跌跤,我的腳險些要滑倒,
4 Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
因我看見惡人安寧幸福,就對驕橫的人心生嫉妒。
5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
原來他們總沒有受過重創,所以他們的身體健康肥胖;
6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
他們沒有別人所受的憂傷,也沒有常人所遭遇的災殃。
7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
故此,驕傲纏繞他們相似項鍊,殘暴遮蔽他們有如衣衫。
8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
他們的邪惡,出自肥胖的心田,讓他們自己的惡念,肆意氾濫。
9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
他們譏諷嘲弄,言惡語狂,他們欺壓恐嚇蠻橫倔強;
10 Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
用自己的口褻瀆上天,以自己的舌詆毀塵寰。
11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
因此我的百姓向他們依歸,滿口啜飲由他們供給的水,
12 Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
且說:天主豈能知悉,難道至高者能理會?
13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
看,這些人為非作歹,常享平安,積存錢財,
14 Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
的確,我白白清心寡欲,我徒然洗手表白無辜。
15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
我時時遭受鞭擊,也天天遇到責斥。
16 Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
我若想:我說話若與他們相同,就等於放棄與您子民為同宗。
17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
我愈設法了解這事,我愈覺得神妙莫測。
18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
直到我接近天主的奧妙,直到我注意他們的結果。
19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
您的確將他們置於坡路,讓他們滑倒於消滅之途。
20 Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
他們瞬息之間變得如此悽涼,他們因受驚過度而從此滅亡。
21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
上主,世人睡醒,怎樣了解夢境;您醒時,也怎樣看他們的幻影。
22 nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
幾時我的心靈遭受酸苦,刺痛也會進入我的肺腑。
23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
原來是我愚昧毫無理性,在您面前竟燃好像畜牲。
24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
但以後,我要常與您同處,您已經握住了我的右手。
25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
您要以您的聖訓來領導我,最後引我進入您的榮耀。
26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
在天上除您以外,為我還能有誰﹖在地上除您以外,為我一無所喜。
27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
我的肉身和我的心靈,雖以憔瘁;天主卻永是我心的福分和磐石。
28 Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
看,遠離您的人必將趨於沉淪。您必消滅一切背棄您的人民。 親近天主對我是多麼的美好:只有上主天主是我的避難所。我要在熙雍女子門前,把您一切的工程宣傳。

< Zaburi 73 >