< Zaburi 72 >

1 Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
Para Salomón. Oh Dios, entrega al Rey tu juicio, y tu justicia al Hijo del Rey;
2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
para que Él gobierne a tu pueblo con justicia, y a los humildes tuyos con equidad.
3 Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
Los montes traerán al pueblo la paz; y los collados, la justicia.
4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
Él defenderá a los humildes del pueblo, Él salvará a los hijos de los pobres, y aplastará al opresor.
5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
Permanecerá como el sol, y como la luna, de generación en generación.
6 Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
Descenderá, como lluvia, sobre el prado segado, como las aguas que riegan la tierra.
7 Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
En sus días florecerá la justicia, y abundará la paz mientras dure la luna.
8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
Y Él dominará de mar a mar, y desde el Río hasta los confines de la tierra.
9 Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
Ante Él se prosternarán sus enemigos, y sus adversarios lamerán el polvo.
10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
Los reyes de Tarsis y de las islas le ofrecerán tributos; los reyes de Arabia y de Sabá le traerán presentes.
11 Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
Y lo adorarán los reyes todos de la tierra; todas las naciones le servirán.
12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
Pues Él librará al que clama desvalido, y al mísero que no tiene amparo.
13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
Se compadecerá del necesitado y del pobre, y a los indigentes salvará la vida,
14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
los libertará del daño y de la opresión, y la sangre de ellos será preciosa a sus ojos.
15 Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
Por eso vivirá; y le darán del oro de Arabia, orarán siempre a causa de Él; sin cesar le bendecirán.
16 Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
Habrá abundancia de trigo en la tierra; en las cumbres de los montes ondeará su fruto como el Líbano; y florecerán los habitantes de las ciudades como la grama del campo.
17 Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
Su nombre será para siempre bendito, mientras dure el sol permanecerá el nombre suyo; y serán benditas en Él todas las tribus de la tierra; todas las naciones lo proclamarán bienaventurado.
18 Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
Bendito sea Yahvé, Dios de Israel, único que hace maravillas;
19 Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
y bendito sea por siempre su glorioso Nombre; llénese de su gloria toda la tierra. ¡Así sea; así sea!
20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.
Fin de las oraciones de David, hijo de Jesé.

< Zaburi 72 >