< Zaburi 72 >

1 Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
Psalmus, In Salomonem.
2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
Deus iudicium tuum regi da: et iustitiam tuam filio regis: Iudicare populum tuum in iustitia, et pauperes tuos in iudicio.
3 Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
Suscipiant montes pacem populo: et colles iustitiam.
4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
Iudicabit pauperes populi, et salvos faciet filios pauperum: et humiliabit calumniatorem.
5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
Et permanebit cum Sole, et ante Lunam, in generatione et generationem.
6 Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
Descendet sicut pluvia in vellus: et sicut stillicidia stillantia super terram.
7 Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
Orietur in diebus eius iustitia, et abundantia pacis: donec auferatur luna.
8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
Et dominabitur a mari usque ad mare: et a flumine usque ad terminos orbis terrarum.
9 Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
Coram illo procident Aethiopes: et inimici eius terram lingent.
10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
Reges Tharsis, et insulae munera offerent: reges Arabum, et Saba dona adducent:
11 Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
Et adorabunt eum omnes reges terrae: omnes gentes servient ei:
12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
Quia liberabit pauperem a potente: et pauperem, cui non erat adiutor.
13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
Parcet pauperi et inopi: et animas pauperum salvas faciet.
14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
Ex usuris et iniquitate redimet animas eorum: et honorabile nomen eorum coram illo.
15 Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
Et vivet, et dabitur ei de auro Arabiae, et adorabunt de ipso semper: tota die benedicent ei.
16 Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
Et erit firmamentum in terra in summis montium, superextolletur super Libanum fructus eius: et florebunt de civitate sicut foenum terrae.
17 Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
Sit nomen eius benedictum in saecula: ante Solem permanet nomen eius. Et benedicentur in ipso omnes tribus terrae: omnes gentes magnificabunt eum.
18 Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
Benedictus Dominus Deus Israel, qui facit mirabilia solus:
19 Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
Et benedictum nomen maiestatis eius in aeternum: et replebitur maiestate eius omnis terra: fiat, fiat.
20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.

< Zaburi 72 >