< Zaburi 72 >
1 Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
神よねがはくは汝のもろもろの審判を王にあたへ なんぢの義をわうの子にあたへたまへ
2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
かれは義をもてなんぢの民をさばき公平をもて苦しむものを鞫かん
3 Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
義によりて山と岡とは民に平康をあたふべし
4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
かれは民のくるしむ者のために審判をなし乏しきものの子輩をすくひ虐ぐるものを壞きたまはん
5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
かれらは日と月とのあらんかぎり世々おしなべて汝をおそるべし
6 Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
かれは苅とれる牧にふる雨のごとく地をうるほす白雨のごとくのぞまん
7 Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
かれの世にただしき者はさかえ平和は月のうするまで豊かならん
8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
またその政治は海より海にいたり河より地のはてにおよぶべし
9 Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
野にをる者はそのまへに屈み そり仇は塵をなめん
10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
タルシシおよび島々の王たちは貢ををさめ シバとセバの王たちは禮物をささげん
11 Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
もろもろの王はそのまへに俯伏し もろもろの國はかれにつかへん
12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
かれは乏しき者をその叫ぶときにすくひ 助けなき苦しむ者をたすけ
13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
弱きものと乏しき者とをあはれみ乏しきものの霊魂をすくひ
14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
かれらのたましひを暴虐と強暴とよりあがなひたまふ その血はみまへに貴かるべし
15 Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
かれらは存ふべし 人はシバの黄金をささげてかれのために恒にいのり終日かれをいははん
16 Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
國のうち五穀ゆたかにしてその實はレバノンのごとく山のいただきにそよぎ 邑の人々は地の草のごとく榮ゆべし
17 Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
かれの名はつねにたえず かれの名は日の久しきごとくに絶ることなし 人はかれによりて福祉をえん もろもろの國はかれをさいはひなる者ととなへん
18 Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
ただイスラエルの神のみ奇しき事跡をなしたまへり 神ヱホバはほむべきかな
19 Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
その榮光の名はよよにほむべきかな全地はその榮光にて滿べしアーメン アーメン
20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.
ヱッサイの子ダビデの祈はをはりぬ