< Zaburi 72 >

1 Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
Psaume pour Salomon.
2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
Dieu, donnez votre jugement au roi; et votre justice au fils du roi.
3 Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
Que les montagnes reçoivent la paix pour le peuple, et les collines la justice.
4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
Il jugera les pauvres du peuple; il sauvera les fils des pauvres, et il humiliera le calomniateur.
5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
Il subsistera avec le soleil et devant la lune, dans toutes les générations.
6 Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
Il descendra comme la pluie sur une toison; et comme des eaux qui tombent goutte à goutte sur la terre.
7 Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
Dans ses jours s’élèvera la justice, et une abondance de paix: jusqu’à ce que la lune disparaisse entièrement.
8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
Et il dominera depuis une mer jusqu’à une autre mer, et depuis un fleuve jusqu’aux limites de la terre.
9 Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
Devant lui se prosterneront les Éthiopiens; et ses ennemis lécheront la poussière.
10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
Les rois de Tharsis et les îles lui offriront des présents; des rois d’Arabie et de Saba lui apporteront des dons;
11 Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
Et tous les rois de la terre l’adoreront: toutes les nations le serviront;
12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
Parce qu’il délivrera le pauvre du puissant; et le pauvre qui n’avait point d’aide.
13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
Il traitera avec ménagement le pauvre et l’homme sans ressource; et il sauvera les âmes des pauvres.
14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
Des usures et de l’iniquité il rachètera leurs âmes; et honorable sera leur nom devant lui.
15 Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
Et il vivra, et on lui donnera de l’or de l’Arabie, et on adorera toujours à son sujet: tout le jour on le bénira.
16 Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
Et il y aura du froment sur la terre, sur des sommets de montagnes; au-dessus du Liban s’élèvera son fruit: et les habitants de la cité fleuriront comme l’herbe de la terre.
17 Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
Que son nom soit béni dans les siècles; avant le soleil subsiste son nom.
18 Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
Béni le Seigneur, le Dieu d’Israël, qui fait des merveilles seul;
19 Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
Et béni le nom de sa majesté éternellement: et toute la terre en sera remplie: ainsi soit, ainsi soit.
20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.
Sont finies les louanges de David, fils de Jessé.

< Zaburi 72 >