< Zaburi 72 >
1 Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
Af Salomo. Gud, giv Kongen din ret, Kongesønnen din retfærd,
2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
saa han dømmer dit Folk med Retfærdighed og dine arme med Ret!
3 Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
Da bærer Bjerge og Høje Fred for Folket i Retfærd.
4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
De arme blandt Folket skaffer han Ret, han bringer de fattige Frelse, og han slaar Voldsmanden ned.
5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
Han skal leve, saa længe Solen lyser og Maanen skinner, fra Slægt til Slægt.
6 Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
Han kommer som Regn paa slagne Enge, som Regnskyl, der væder Jorden;
7 Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
i hans Dage blomstrer Retfærd, og dyb Fred raader, til Maanen forgaar.
8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
Fra Hav til Hav skal han herske, fra Floden til Jordens Ender;
9 Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
hans Avindsmænd bøjer Knæ for ham, og hans Fjender slikker Støvet;
10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
Konger fra Tarsis og fjerne Strande frembærer Gaver, Sabas og Sebas Konger kommer med Skat;
11 Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
alle Konger skal bøje sig for ham, alle Folkene være hans Tjenere.
12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
Thi han skal redde den fattige, der skriger om Hjælp, den arme, der savner en Hjælper,
13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
ynkes over ringe og fattig og frelse fattiges Sjæle;
14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
han skal fri deres Sjæle fra Uret og Vold, deres Blod er dyrt i hans Øjne.
15 Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
Maatte han leve og Guld fra Saba gives ham! De skal bede for ham bestandig, velsigne ham Dagen igennem.
16 Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
Korn skal der være i Overflod i Landet, paa Bjergenes Top; som Libanon skal dets Afgrøde bølge og Folk spire frem af Byen som Jordens Urter.
17 Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
Velsignet være hans Navn evindelig, hans Navn skal leve, mens Solen skinner. Ved ham skal man velsigne sig, alle Folk skal prise ham lykkelig!
18 Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
Lovet være Gud HERREN, Israels Gud, som ene gør Undergerninger,
19 Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
og lovet være hans herlige Navn evindelig; al Jorden skal fyldes af hans Herlighed. Amen, Amen!
20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.
Her ender Davids, Isajs Søns, Bønner.