< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
J'ai cherché en toi mon refuge, ô Éternel; Que mon espoir ne soit jamais déçu!
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Dans ta justice, délivre-moi, retire-moi du danger; Incline ton oreille vers moi, et sauve-moi!
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Sois mon rocher, la retraite Où je puisse me réfugier en tout temps! Tu as donné des ordres pour que je sois sauvé; Car tu es mon rocher et ma forteresse.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Mon Dieu, délivre-moi des mains du méchant, Des mains de l'homme inique et de l'oppresseur!
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
Car tu es mon espérance, ô Seigneur, Éternel! C'est en toi que je me confie depuis ma jeunesse.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
Je me suis appuyé sur toi dès ma naissance; C'est toi qui m'as tiré du sein de ma mère! Tu es l'objet de mes louanges en tout temps.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
Je suis, pour plusieurs, un sujet d'étonnement; Mais toi, tu es ma forte citadelle.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Que ma bouche soit pleine de ta louange. Et qu'elle te glorifie chaque jour!»
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Ne me rejette pas au temps de ma vieillesse; Quand ma force s'en va, ne m'abandonne point!
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
Car mes ennemis parlent de moi; Ceux qui guettent ma vie conspirent ensemble,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
Disant: «Dieu l'a abandonné; Poursuivez-le, saisissez-le; Car il n'y a personne pour le délivrer!»
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
Dieu! Ne t'éloigne pas de moi! Mon Dieu, accours à mon aide!
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Que ceux qui en veulent à ma vie Rougissent de honte et qu'ils périssent! Que ceux qui cherchent ma perte Soient couverts d'opprobre et de confusion!
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
Mais moi, j'espérerai en tout temps, Et je te louerai toujours davantage.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
Ma bouche célébrera chaque jour Ta justice et tes délivrances. Sans jamais parvenir à énumérer tes bienfaits.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
Je raconterai partout tes grandes oeuvres, Seigneur, Éternel! C'est ta justice seule que je célébrerai.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
Dieu, tu m'as instruit dès ma jeunesse. Et jusqu'à ce jour j'ai fait connaître tes oeuvres merveilleuses,
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
C'est pourquoi, jusqu'à la vieillesse. Jusqu'à la blanche vieillesse, Dieu, ne m'abandonne pas, Afin que je révèle la vigueur de ton bras à la génération nouvelle, Et ta puissance à tous ceux qui naîtront!
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Ta justice, ô Dieu, atteint jusqu'au ciel! Tu as accompli de grandes oeuvres. Dieu, qui est semblable à toi?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Après m'avoir fait passer par des détresses Et des maux sans nombre. Tu m'as de nouveau rendu la vie, Et tu m'as fait remonter des abîmes de la terre!
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Tu accroîtras ma grandeur, Et tu me consoleras encore.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
Aussi, je te célébrerai sur les cordes de la lyre; Je chanterai ta fidélité, ô mon Dieu! Je psalmodierai en ton honneur sur la harpe, ô Saint d'Israël!
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
Mes lèvres, et mon âme que tu as rachetée, Entonneront des chants de joie. Quand je psalmodierai à ta gloire.
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
Ma langue aussi, chaque jour, redira ta justice; Car ils seront confus, ils rougiront. Ceux qui souhaitent ma ruine!

< Zaburi 71 >