< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
Eternel! je me suis retiré vers toi, fais que je ne sois jamais confus.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Délivre-moi par ta justice, et me garantis: incline ton oreille vers moi, et me mets en sûreté.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Sois-moi pour un rocher de retraite, afin que je m'y puisse toujours retirer; tu as donné ordre de me mettre en sûreté; car tu es mon rocher, et ma forteresse.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Mon Dieu! délivre-moi de la main du méchant, de la main du pervers, et de l'oppresseur.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
Car tu es mon attente, Seigneur Eternel! [et] ma confiance dès ma jeunesse.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
J'ai été appuyé sur toi dès le ventre [de ma mère]; c'est toi qui m'as tiré hors des entrailles de ma mère; tu es le sujet continuel de mes louanges.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
J'ai été à plusieurs comme un monstre; mais tu es ma forte retraite.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Que ma bouche soit remplie de ta louange, et de ta magnificence chaque jour.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Ne me rejette point au temps de ma vieillesse; ne m'abandonne point maintenant que ma force est consumée.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
Car mes ennemis ont parlé de moi, et ceux qui épient mon âme ont pris conseil ensemble;
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
Disant: Dieu l'a abandonné; poursuivez-le, et le saisissez; car il n'y a personne qui le délivre.
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
Ô Dieu! ne t'éloigne point de moi; mon Dieu hâte-toi de venir à mon secours.
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Que ceux qui sont ennemis de mon âme soient honteux et défaits; et que ceux qui cherchent mon mal soient enveloppés d'opprobre et de honte.
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
Mais moi je vivrai toujours en espérance en toi, et je te louerai tous les jours davantage.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
Ma bouche racontera chaque jour ta justice, [et] ta délivrance, bien que je n'en sache point le nombre.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
Je marcherai par la force du Seigneur Eternel; je raconterai ta seule justice.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
Ô Dieu! tu m'as enseigné dès ma jeunesse, et j'ai annoncé jusques à présent tes merveilles.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
[Je les ai annoncées] jusqu’à la vieillesse, même jusques à la vieillesse toute blanche; ô Dieu! ne m'abandonne point jusqu’à ce que j'aie annoncé ton bras à cette génération, et ta puissance à tous ceux qui viendront après.
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Car ta justice, ô Dieu! est haut élevée, parce que tu as fait de grandes choses. Ô Dieu qui est semblable à toi?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Qui m'ayant fait voir plusieurs détresses et plusieurs maux, m'as de nouveau rendu la vie, et m'as fait remonter hors des abîmes de la terre?
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Tu accroîtras ma grandeur, et tu me consoleras encore.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
Aussi, mon Dieu! je te célébrerai pour l'amour de ta vérité avec l'instrument de la musette; ô Saint d'Israël, je te psalmodierai avec la harpe.
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
Mes lèvres et mon âme, que tu auras rachetée, chanteront de joie, quand je te psalmodierai.
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
Ma langue aussi discourra chaque jour de ta justice, parce que ceux qui cherchent mon mal seront honteux et rougiront.

< Zaburi 71 >