< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
En toi, Seigneur, je m’abrite! Puissé-je n’être jamais déçu!
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Dans ta justice, sauve-moi, retire-moi du danger; incline vers moi ton oreille, et viens à mon secours.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Sois pour moi un rocher tutélaire, toujours accessible; fais-toi une loi de me prêter assistance, car tu es bien mon rocher et ma citadelle.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Mon Dieu, délivre-moi de la main du méchant, de la poigne de l’homme inique et violent.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
Car tu es mon espoir, Seigneur Dieu, ma sauvegarde depuis ma jeunesse.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
Sur toi je m’appuie depuis mon enfance; c’est toi qui m’as tiré des entrailles de ma mère: tu es l’objet constant de mes louanges.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
Pour beaucoup, j’ai l’air d’un insigne prodige; mais toi, tu es mon solide abri.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
J’Ai la bouche pleine de louanges; sans cesse je prône ta gloire.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Ne me rejette pas au temps de ma vieillesse; alors que ma vigueur est épuisée, ne m’abandonne point.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
Car mes ennemis s’entretiennent de moi, ceux qui guettent ma vie se concertent ensemble.
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
Ils disent: "Dieu l’a délaissé, courez-lui sus, empoignez-le, car il n’est personne pour le sauver!"
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
O Dieu, ne te tiens pas éloigné de moi; mon Dieu, hâte-toi de me venir en aide.
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Qu’ils soient confondus, réduits à néant, ceux qui me vouent leur haine; qu’ils soient enveloppés de honte et d’ignominie, ceux qui cherchent mon malheur!
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
Pour moi, je serai toujours plein d’espoir, et j’ajouterai encore à toutes tes louanges.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
Ma bouche proclamera ton équité, tout le temps, ta protection; car je suis impuissant à tout énumérer.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
Je me présenterai avec tes hauts faits, ô Seigneur Dieu, je célébrerai ta justice à toi seul.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
O Dieu, tu m’as appris à les connaître dès ma jeunesse, et jusqu’à ce jour, j’annonce tes merveilles.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
Aussi, jusque dans ma vieillesse et sous les cheveux blancs, tu ne m’abandonneras pas, ô Dieu, pour que je puisse révéler ta force à ma génération, ta puissance à toute la postérité.
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Ta justice, ô Dieu, atteint, en effet, jusqu’au ciel: tu accomplis de grandes choses: ô Dieu, qui est comme toi?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Toi qui m’as fait voir des épreuves nombreuses et cruelles, à nouveau tu me rendras la vie, à nouveau tu me feras remonter du fond des abîmes.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Tu accroîtras ma grandeur, et tu te retourneras vers moi pour me consoler.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
En retour, moi, je te louerai au son du luth, pour ta bonté fidèle, ô mon Dieu; je te chanterai avec la harpe, ô Saint d’Israël!
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
Mes lèvres entonneront des cantiques, lorsque je voudrai te célébrer, ainsi que mon âme qui te doit sa délivrance.
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
Oui, ma langue proclamera ta justice tout le long du jour, car ils auront été confondus, couverts de honte, ceux qui voulaient mon malheur.

< Zaburi 71 >