< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
In Thee, O Jehovah, I have trusted, Let me not be ashamed to the age.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
In Thy righteousness Thou dost deliver me, And dost cause me to escape, Incline unto me Thine ear, and save me.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Be to me for a rock — a habitation, To go in continually, Thou hast given command to save me, For my rock and my bulwark [art] Thou.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
O my God, cause me to escape From the hand of the wicked, From the hand of the perverse and violent.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
For Thou [art] my hope, O Lord Jehovah, My trust from my youth.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
By Thee I have been supported from the womb, From my mother's bowels Thou dost cut me out, In Thee [is] my praise continually.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
As a wonder I have been to many, And Thou [art] my strong refuge.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Filled is my mouth [with] Thy praise, All the day [with] Thy beauty.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Cast me not off at the time of old age, According to the consumption of my power forsake me not.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
For mine enemies have spoken against me, And those watching my soul have taken counsel together,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
Saying, 'God hath forsaken him, Pursue and catch him, for there is no deliverer.'
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
O God, be not far from me, O my God, for my help make haste.
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
They are ashamed, they are consumed, Who are opposing my soul, They are covered [with] reproach and blushing, Who are seeking my evil,
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
And I continually do wait with hope, And have added unto all Thy praise.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
My mouth recounteth Thy righteousness, All the day Thy salvation, For I have not known the numbers.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
I come in the might of the Lord Jehovah, I mention Thy righteousness — Thine only.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
God, Thou hast taught me from my youth, And hitherto I declare Thy wonders.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
And also unto old age and grey hairs, O God, forsake me not, Till I declare Thy strength to a generation, To every one that cometh Thy might.
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
And Thy righteousness, O God, [is] unto the heights, Because Thou hast done great things, O God, who [is] like Thee?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Because Thou hast showed me many and sad distresses, Thou turnest back — Thou revivest me, And from the depths of the earth, Thou turnest back — Thou bringest me up.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Thou dost increase my greatness, And Thou surroundest — Thou comfortest me,
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
I also thank Thee with a vessel of psaltery, Thy truth, O my God, I sing to Thee with a harp, O Holy One of Israel,
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
My lips cry aloud when I sing praise to Thee, And my soul that Thou hast redeemed,
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
My tongue also all the day uttereth Thy righteousness, Because ashamed — because confounded, Have been those seeking my evil!

< Zaburi 71 >