< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
In you O Yahweh I have taken refuge may not I be ashamed for ever.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
In righteousness your you will rescue me and you will deliver me incline to me ear your and save me.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Become of me - a rock a dwelling place to go continually you have given command to save me for [are] rock my and stronghold my you.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
O God my deliver me from [the] hand of [the] wicked from [the] hand of [the] wrongdoer and [the] ruthless.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
For you [are] hope my O Lord Yahweh confidence my since youth my.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
On you - I have supported myself from [the] womb from [the] inward parts of mother my you [were [the] one who] cut off me [is] in you praise my continually.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
Like a portent I have become for many [people] and you [are] refuge of my strength.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
It is filled mouth my praise your all the day splendor your.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
May not you cast away me to a time of old age when fails strength my may not you forsake me.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
For they have spoken enemies my of me and [those who] watch of life my they have consulted together.
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
Saying God he has forsaken him pursue and seize him for there not [is] a deliverer.
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
O God may not you be far from me O God my to help my (make haste! *Q(K)*)
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
May they be ashamed may they come to an end [the] accusers of self my may they cover themselves reproach and ignominy [those who] seek harm my.
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
And I continually I will wait and I will add to all praise your.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
Mouth my - it will recount righteousness your all the day salvation your for not I know numbers.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
I will come with [the] mighty deeds of [the] Lord Yahweh I will bring to remembrance righteousness your to alone you.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
O God you have taught me since youth my and until now I declare wonders your.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
And also until old age - and grey hair O God may not you forsake me until I will declare strength your to a generation to every [one who] he will come might your.
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
And righteousness your O God [is] to [the] height who you have done great [things] O God who? [is] like you.
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Who (you have made see me *Q(K)*) troubles many and calamities you will return (you will preserve alive me *Q(K)*) and from [the] depths of the earth you will return you will bring up me.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
May you increase - greatness my and may you turn may you comfort me.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
Also I - I will praise you with an instrument of a lyre faithfulness your O God my I will make music to you with a harp O holy [one] of Israel.
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
They will sing for joy lips my if I will make music to you and self my which you have redeemed.
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
Also tongue my all the day it will utter righteousness your for they are ashamed for they are abashed [those who] seek harm my.

< Zaburi 71 >