< Zaburi 71 >
1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
By David, [a Psalm sung by] the sons of Jonadab, and the first that were taken captive. O Lord, I have hoped in thee: let me never be put to shame.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
In thy righteousness deliver me and rescue me: incline thine ear to me, and save me.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Be to me a protecting God, and a strong hold to save me: for thou art my fortress and my refuge.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Deliver me, O my God, from the hand of the sinner, from the hand of the transgressor and unjust man.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
For thou art my support, O Lord; O Lord, [thou art] my hope from my youth.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
On thee have I been stayed from the womb: from the belly of my mother thou art my protector: of thee is my praise continually.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
I am become as it were a wonder to many: but thou art [my] strong helper.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Let my mouth be filled with praise, that I may hymn thy glory, [and] thy majesty all the day.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Cast me not off at the time of old age; forsake me not when my strength fails.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
For mine enemies have spoken against me; and they that lay wait for my soul have taken counsel together,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
saying, God has forsaken him: persecute ye and take him; for there is none to deliver [him].
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
O God, go not far from me, O my God, draw nigh to my help.
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Let those that plot against my soul be ashamed and utterly fail: let those that seek my hurt be clothed with shame and dishonour.
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
But I will hope continually, and will praise thee more and more.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
My mouth shall declare thy righteousness openly, [and] thy salvation all the day; for I am not acquainted with the affairs [of men].
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
I will go on in the might of the Lord: O Lord, I will make mention of thy righteousness only.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
O God, thou hast taught me from my youth, and until now will I declare thy wonders;
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
even until I am old and advanced in years. O God, forsake me not; until I shall have declared thine arm to all the generation that is to come:
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
even thy power and thy righteousness, O God, up to the highest [heavens, even] the mighty works which thou has done: O God, who is like to thee?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
What afflictions many and sore hast thou shewed me! yet thou didst turn and quicken me, and broughtest me again from the depths of the earth.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Thou didst multiply thy righteousness, and didst turn and comfort me, and broughtest me again out of the depths of the earth.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
I will also therefore give thanks to thee, O God, [because of] thy truth, on an instrument of psalmody: I will sing psalms to thee on the harp, O Holy One of Israel.
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
My lips shall rejoice when I sing to thee; and my soul, which thou hast redeemed.
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
Moreover also my tongue shall dwell all the day upon thy righteousness; when they shall be ashamed and confounded that seek my hurt.