< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
In you, LORD, I take refuge. Never let me be disappointed.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Deliver me in your righteousness, and rescue me. Turn your ear to me, and save me.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Be to me a rock of refuge to which I may always go. Give the command to save me, for you are my rock and my fortress.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Rescue me, my God, from the hand of the wicked, from the hand of the unrighteous and cruel man.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
For you are my hope, Lord GOD, my confidence from my youth.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
I have relied on you from the womb. You are he who took me out of my mother’s womb. I will always praise you.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
I am a marvel to many, but you are my strong refuge.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
My mouth shall be filled with your praise, with your honor all day long.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Do not reject me in my old age. Do not forsake me when my strength fails.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
For my enemies talk about me. Those who watch for my soul conspire together,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
saying, “God has forsaken him. Pursue and take him, for no one will rescue him.”
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
God, do not be far from me. My God, hurry to help me.
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Let my accusers be disappointed and consumed. Let them be covered with disgrace and scorn who want to harm me.
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
But I will always hope, and will add to all of your praise.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
My mouth will tell about your righteousness, and of your salvation all day, though I do not know its full measure.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
I will come with the mighty acts of the Lord GOD. I will make mention of your righteousness, even of yours alone.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
God, you have taught me from my youth. Until now, I have declared your wondrous works.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
Yes, even when I am old and gray-haired, God, do not forsake me, until I have declared your strength to the next generation, your might to everyone who is to come.
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
God, your righteousness also reaches to the heavens. You have done great things. God, who is like you?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
You, who have shown us many and bitter troubles, you will let me live. You will bring us up again from the depths of the earth.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Increase my honor and comfort me again.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
I will also praise you with the harp for your faithfulness, my God. I sing praises to you with the lyre, Holy One of Israel.
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
My lips shall shout for joy! My soul, which you have redeemed, sings praises to you!
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
My tongue will also talk about your righteousness all day long, for they are disappointed, and they are confounded, who want to harm me.

< Zaburi 71 >