< Zaburi 71 >
1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
HERRE, jeg lider på dig, lad mig aldrig i evighed skuffes.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Frels mig og udfri mig i din Retfærdighed, du bøjede dit Øre til mig;
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
red mig og vær mig en Tilflugtsklippe, en Klippeborg til min Frelse; thi du er min Klippe og Borg!
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Min Gud, fri mig ud af gudløses Hånd, af Niddings og Voldsmands Kløer;
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
thi du er mit Håb, o Herre! Fra min Ungdom var HERREN min Tillid;
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
fra Moders Skød har jeg støttet mig til dig, min Forsørger var du fra Moders Liv, dig gælder altid min Lovsang.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
For mange står jeg som mærket af Gud, men du er min stærke Tilflugt;
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
min Mund er fuld af din Lovsang, af din Ære Dagen lang.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Forkast mig ikke i Alderdommens Tid og svigt mig ikke, nu Kraften svinder;
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
thi mine Fjender taler om mig, de der lurer på min Sjæl, holder Råd:
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
"Gud har svigtet ham! Efter ham! Grib ham, thi ingen frelser!"
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
Gud, hold dig ikke borte fra mig, il mig til Hjælp, min Gud;
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
lad dem blive til Skam og Skændsel, dem, der står mig imod, lad dem hylles i Spot og Spe, dem, der vil mig ondt!
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
Men jeg, jeg vil altid håbe, blive ved at istemme din Pris;
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
min Mund skal vidne om din Retfærd, om din Frelse Dagen lang; thi jeg kender ej Ende derpå.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
Jeg vil minde om den Herre HERRENs Vælde, lovsynge din Retfærd, kun den alene.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
Gud, du har vejledt mig fra min Ungdom af, dine Undere har jeg forkyndt til nu;
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
indtil Alderdommens Tid og de grånende Hår svigte du mig ikke, o Gud. End skal jeg prise din Arm for alle kommende Slægter.
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Din Vælde og din Retfærdighed når til Himlen, o Gud; du, som øvede store Ting, hvo er din Lige, Gud?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Du, som lod os skue mange fold Trængsel og Nød, du kalder os atter til Live og drager os atter af Jordens Dyb;
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
du vil øge min Storhed og atter trøste mig.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
Til Gengæld vil jeg til Harpespil prise din Trofasthed, min Gud, lege på Citer for dig, du Israels Hellige;
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
juble skal mine Læber - ja, jeg vil lovsynge dig og min Sjæl, som du udløste;
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
også min Tunge skal Dagen igennem forkynde din Retfærd, thi Skam og Skændsel får de, som vil mig ilde.