< Zaburi 70 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa; Ee Bwana, njoo hima unisaidie.
למנצח לדוד להזכיר אלהים להצילני יהוה לעזרתי חושה׃
2 Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu.
יבשו ויחפרו מבקשי נפשי יסגו אחור ויכלמו חפצי רעתי׃
3 Wale waniambiao, “Aha! Aha!” warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.
ישובו על עקב בשתם האמרים האח האח׃
4 Lakini wote wakutafutao washangilie na kukufurahia, wale wapendao wokovu wako siku zote waseme, “Mungu na atukuzwe!”
ישישו וישמחו בך כל מבקשיך ויאמרו תמיד יגדל אלהים אהבי ישועתך׃
5 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji; Ee Mungu, unijie haraka. Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu; Ee Bwana, usikawie.
ואני עני ואביון אלהים חושה לי עזרי ומפלטי אתה יהוה אל תאחר׃

< Zaburi 70 >