< Zaburi 69 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni.
聖歌隊の指揮者によってゆりの花のしらべにあわせてうたわせたダビデの歌 神よ、わたしをお救いください。大水が流れ来て、わたしの首にまで達しました。
2 Ninazama kwenye vilindi vya matope, pasipo mahali pa kukanyaga, Nimefika kwenye maji makuu, mafuriko yamenigharikisha.
わたしは足がかりもない深い泥の中に沈みました。わたしは深い水に陥り、大水がわたしの上を流れ過ぎました。
3 Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.
わたしは叫びによって疲れ、わたしののどはかわき、わたしの目は神を待ちわびて衰えました。
4 Wale wanaonichukia bila sababu ni wengi kuliko nywele za kichwa changu; wengi ni adui kwangu bila sababu, wale wanaotafuta kuniangamiza. Ninalazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.
ゆえなく、わたしを憎む者はわたしの頭の毛よりも多く、偽ってわたしの敵となり、わたしを滅ぼそうとする者は強いのです。わたしは盗まなかった物をも償わなければならないのですか。
5 Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu, wala hatia yangu haikufichika kwako.
神よ、あなたはわたしの愚かなことを知っておられます。わたしのもろもろのとがはあなたに隠れることはありません。
6 Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote, wakutumainio wasiaibishwe kwa ajili yangu; wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.
万軍の神、主よ、あなたを待ち望む者がわたしの事によって、はずかしめられることのないようにしてください。イスラエルの神よ、あなたを求める者がわたしの事によって、恥を負わせられることのないようにしてください。
7 Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako, aibu imefunika uso wangu.
わたしはあなたのためにそしりを負い、恥がわたしの顔をおおったのです。
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
わたしはわが兄弟には、知らぬ者となり、わが母の子らには、のけ者となりました。
9 Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila, matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
あなたの家を思う熱心がわたしを食いつくし、あなたをそしる者のそしりがわたしに及んだからです。
10 Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.
わたしが断食をもってわたしの魂を悩ませば、かえってそれによってそしりをうけました。
11 Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.
わたしが荒布を衣とすれば、かえって彼らのことわざとなりました。
12 Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.
わたしは門に座する者の話題となり、酔いどれの歌となりました。
13 Lakini Ee Bwana, ninakuomba, kwa wakati ukupendezao; katika upendo wako mkuu, Ee Mungu, unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
しかし主よ、わたしはあなたに祈ります。神よ、恵みの時に、あなたのいつくしみの豊かなるにより、わたしにお答えください。
14 Uniokoe katika matope, usiniache nizame; niokoe na hao wanichukiao, kutoka kwenye vilindi vya maji.
あなたのまことの救により、わたしを泥の中に沈まぬよう助け出してください。わたしを憎む者から、また深い水からわたしを助け出してください。
15 Usiache mafuriko yanigharikishe au vilindi vinimeze, au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
大水がわたしの上を流れ過ぎることなく、淵がわたしをのむことなく、穴がその口をわたしの上に閉じることのないようにしてください。
16 Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako; kwa huruma zako nyingi unigeukie.
主よ、あなたのいつくしみの深きにより、わたしにお答えください。あなたのあわれみの豊かなるにより、わたしを顧みてください。
17 Usimfiche mtumishi wako uso wako, uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
あなたの顔をしもべに隠さないでください。わたしは悩んでいるのです。すみやかにわたしにお答えください。
18 Njoo karibu uniokoe, nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
わたしに近く寄って、わたしをあがない、わが敵のゆえにわたしをお救いください。
19 Unajua jinsi ninavyodharauliwa, kufedheheshwa na kuaibishwa, adui zangu wote unawajua.
あなたはわたしの受けるそしりと、恥と、はずかしめとを知っておられます。わたしのあだは皆あなたの前にあります。
20 Dharau zimenivunja moyo na nimekata tamaa, nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata, wa kunituliza, lakini sikumpata.
そしりがわたしの心を砕いたので、わたしは望みを失いました。わたしは同情する者を求めたけれども、ひとりもなく、慰める者を求めたけれども、ひとりも見ませんでした。
21 Waliweka nyongo katika chakula changu na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
彼らはわたしの食物に毒を入れ、わたしのかわいた時に酢を飲ませました。
22 Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego, nayo iwe upatilizo na tanzi.
彼らの前の食卓を網とし、彼らが犠牲をささげる祭を、わなとしてください。
23 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.
彼らの目を暗くして見えなくし、彼らの腰を常に震わせ、
24 Uwamwagie ghadhabu yako, hasira yako kali na iwapate.
あなたの憤りを彼らの上にそそぎ、あなたの激しい怒りを彼らに追いつかせてください。
25 Mahali pao na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
彼らの宿営を荒し、ひとりもその天幕に住まわせないでください。
26 Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi, na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
彼らはあなたが撃たれた者を迫害し、あなたが傷つけられた者をさらに苦しめるからです。
27 Walipize uovu juu ya uovu, usiwaache washiriki katika wokovu wako.
彼らに、罰に罰を加え、あなたの赦免にあずからせないでください。
28 Wafutwe kutoka kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
彼らをいのちの書から消し去って、義人のうちに記録されることのないようにしてください。
29 Mimi niko katika maumivu na dhiki; Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
しかしわたしは悩み苦しんでいます。神よ、あなたの救がわたしを高い所に置かれますように。
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
わたしは歌をもって神の名をほめたたえ、感謝をもって神をあがめます。
31 Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume, zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
これは雄牛または角とひずめのある雄牛にまさって主を喜ばせるでしょう。
32 Maskini wataona na kufurahi: ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
へりくだる者は、これを見て喜べ。神を求める者よ、あなたがたの心を生きかえらせよ。
33 Bwana huwasikia wahitaji wala hadharau watu wake waliotekwa.
主は乏しい者に聞き、その捕われ人をかろしめられないからである。
34 Mbingu na dunia zimsifu, bahari na vyote viendavyo ndani yake,
天と地は主をほめたたえ、海とその中に動くあらゆるものは主をほめたたえよ。
35 kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na kuijenga tena miji ya Yuda. Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
神はシオンを救い、ユダの町々を建て直されるからである。そのしもべらはそこに住んでこれを所有し、
36 watoto wa watumishi wake watairithi na wale wote walipendao jina lake wataishi humo.
そのしもべらの子孫はこれを継ぎ、み名を愛する者はその中に住むであろう。

< Zaburi 69 >