< Zaburi 68 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
Naj vstane Bog, naj bodo njegovi sovražniki razkropljeni. Naj tudi tisti, ki ga sovražijo, bežijo pred njim.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Kakor je pregnan dim, tako jih preženi. Kakor se vosek stopi pred ognjem, tako naj bodo zlobni pogubljeni pred prisotnostjo Boga.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
Toda pravični naj bodo veseli, naj se veselijo pred Bogom. Da, naj se silno veselijo.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Prepevajte Bogu, prepevajte hvalnice njegovemu imenu. Povzdigujte njega, ki jaha po nebesih s svojim imenom Jah in se veselite pred njim.
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Oče osirotelim in sodnik vdovam je Bog v svojem svetem prebivališču.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
Bog osamljene postavlja v družine, osvobaja tiste, ki so zvezani z verigami, toda uporni prebivajo v suhi deželi.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
Oh Bog, ko si šel naprej pred svojim ljudstvom, ko si korakal skozi divjino, (Sela)
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
se je zemlja tresla, tudi nebo je kapljalo ob prisotnosti Boga. Celó sam Sinaj je bil premaknjen ob prisotnosti Boga, Izraelovega Boga.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
Ti, oh Bog, si poslal obilen dež, s čimer si potrdil svojo dediščino, ko je bila izmučena.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Tvoja skupnost je prebivala tam. Ti, oh Bog, si od svoje dobrote pripravil za uboge.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
Gospod je dal besedo. Velika je bila skupina teh, ki so jo razglašali.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Kralji vojská so naglo zbežali; tista pa, ki je ostala doma, je razdelila plen.
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
Čeprav si ležala med lonci, boš vendar kakor peruti golobice, [ki sta] pokriti s srebrom in njena peresa z rumenim zlatom.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Ko je Vsemogočni v njej razkropil kralje, je bilo belo kakor sneg na Calmónu.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Božja gora je kakor bašánska gora, visoka gora kakor bašánska gora.
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Zakaj poskakujete, ve visoke gore? To je gora, na kateri želi prebivati Bog; da, Gospod bo na njej prebival na veke.
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Božjih bojnih vozov je dvajset tisoč, celó tisoči angelov. Gospod je med njimi kakor na Sinaju, na svetem kraju.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Ti si se dvignil na visoko, vodil si ujeto ujetništvo. Prejel si darila za ljudi, da, tudi za uporne, da bi med njimi lahko prebival Gospod Bog.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Blagoslovljen bodi Gospod, ki nas dnevno zalaga s koristmi, celó Bog rešitve naše duše. (Sela)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Kdor je naš Bog, je Bog rešitve duše in Bogu, Gospodu, pripadajo izhodi pred smrtjo.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
Toda Bog bo ranil glavo svojih sovražnikov in lasato tême tistega, ki nenehno hodi v svojih prekrških.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
Gospod je rekel: »Ponovno bom privedel iz Bašána, ponovno bom svoje ljudstvo privedel iz morskih globin,
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
da bo tvoje stopalo lahko pomočeno v krvi tvojih sovražnikov in jezik tvojih psov v istem.«
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
Videli so tvoje sprevode, oh Bog, celó sprevode mojega Boga, mojega Kralja, v svetišču.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
Pevci so šli spredaj, igralci na glasbila so sledili zadaj, med njimi so bile gospodične, ki so igrale s tamburini.
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
Blagoslavljajte Boga v skupnostih, celó Gospoda, iz Izraelovega studenca.
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
Tam je majhen Benjamin z njihovim vladarjem, Judovi princi in njihov zbor, Zábulonovi princi in Neftálijevi princi.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Tvoj Bog je zapovedal tvojo moč. Ojačaj, oh Bog, to, kar si izvršil za nas.
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
Zaradi tvojega templja pri Jeruzalemu ti bodo kralji prinašali darila.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Oštej skupino suličarjev, množico bikov s teleti ljudstva, dokler vsakdo sebe ne podredi s koščki srebra. Razkropi ljudstvo, ki se razveseljuje v vojni.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Princi bodo prišli iz Egipta, Etiopija bo svoje roke kmalu iztegnila k Bogu.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
Prepevajte Bogu, ve, zemeljska kraljestva, oh prepevajte hvalnice Gospodu, (Sela)
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
Njemu, ki jaha po nebes nebesih, ki so bila od davnine; glej, poslal je svoj glas in to mogočen glas.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Moč pripišite Bogu. Njegova odličnost je nad Izraelom in njegova moč je v oblakih.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Oh Bog, ti si strašen iz svojih svetih prostorov. Izraelov Bog je ta, ki daje svojemu ljudstvu moč in oblast. Blagoslovljen bodi Bog.