< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
Hiongake t’i Andrianañahare, le hiparaitake o rafelahi’eo; vaho hibioñe aolo’e eo o malaiñe Azeo.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Hambañe ami’ty fampisaohañe hatoeñe, isaoho añe ka; manahake ty fitranaha’ o karafo tantele aolo’ afoo, ty hikoromaha’ o tsivokatseo añatrefan’Añahare.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
Ho ehake o vañoñeo, hirebeke añ’atrefan’Añahare eo, hiriñariña an-kobaiñe.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Misaboa aman’ Añahare, bangò i tahina’ey; onjono i Mpiningitse miranga i montombeiy, Ià ty tahina’e; vaho mitreñà añatrefa’e eo.
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Raem-bode-rae naho mpañomey to amo vantotseo t’i Andrianañahare an-kivoho’e miavake ao.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
Ampimoneñan’ Añahare añ’akiba ao ty jorý; akare’e mb’an-kavokarañe o rinohio; fe mitobok’ an-tane kirikintàñe ao o mpitrabikeo.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
O Andrianañahare, ie niaoloa’o ondati’oo, ie nihofiha’o firanga i fatram-beiy, Selà
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
niezeñezeñe i taney, nihotrake i likerañey aolo’ i Andrianamboatse, Nihondrahondra ty Sinay añatrefa’ i Abo Tia, Andrianañahare’ Israele eo.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
Nanondraha’o oran-joba, ry Andrianañahare; niventè’o i lova’o navozoy,
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Nitobok’ ao i mpirai-lia’oy, nifahana’o ami’ty havokara’o o rarakeo, ry Andrianamboatse.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
Nitaroñe t’i Talè; mitozantoza o rakemba mitalily i entañeio.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Nitriban-day mb’eo o mpanjakan- dahindefoñeo! Nivoratsake; le ho zarae’ i tambatse an-kiboho’e ao o kinopakeo,
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
ie mandre am-bàlan’añondry ao, le manahake ty elan-deho misarom-bola-foty; mimilemiletse volamena o volo’eo.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Ie nampivarakai’ i El-Sadai i mpanjaka rey, le niavy an-Tsalmone ty oram-panala.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Vohin’ Añahare ty vohy Basane; vohitse lako-lengo’e ty haboa’ i Basane;
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Inoñe ty ikiraña’ areo ry haboañe maro-lengo’eo, i vohitse nirien’Añahare himoneña’ey? Eka himoneñe ao nainai’e t’Iehovà.
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Añ’ale’ale o sareten’ Añahareo, arivo-añ’arivo’e; ama’e ao an-kamasiña’e t’i Talè manahake e Sinay añe.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Nionjoñe añ’abo eñe irehe, nikozozote’o an-drohy o fandrohizañeo, nandrambe ravoravo am’ondatio, vaho amo mpiolao, himoneña’ Ià, Andrianañahare.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Andriañeñe t’i Talè mpivave o kilankan-tikañeo boak’andro, i Andrianañaharem- pandrombahantikañey. Selà
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Andrianañaharem-pañaha an-tika t’i Andrianamboatse; Toe a Iehovà Talè ty famotsorañe an-kavilasy.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
Le hanorotoro ty loha’ o rafelahi’eo t’i Andrianañahare, ty kovo-doha minankanankañe amo hakeo’eo.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
Hoe t’i Talè: Hampoliko o e Basaneo, hahereko boak’ an-keraheran-driak’ ao,
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
Ho demohem-pandia’o an-dio o rafelahi’oo, hanañ’anjara an-dion-drafilahy ka o lelan’ amboa’oo.
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
Fa niisa’ iareo o fañaveloa’oo ry Andrianañahare, ty fionjonan’ Añahareko, toe i Mpanjakakoy, mb’amy miavakey ao.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
Miaolo o mpisaboo, manonjohy o mpititikeo; añivo’e ao o somondrara mampikantsankantsàñe o kantsàñeo:
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
Andriaño am-pivory ao t’i Andrianañahare, i Iehovà boak’am-pigoa­ngoaña’ Israele.
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
Ingo t’i Beniamine tsitso’e, miaolo iareo, o roandria’ Iehodào am-pirimboña’eo, o roandria’ i Zeboloneo, o roandria’ i Naftalio.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Fa linilin’ Añahare’o ty haozara’o; mihaozara! Ry Andrianañahare, nañenefa’o ho anay izay,
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
ty kiboho’o e Ierosalaime añe, ty ibanabanà’ o mpanjakao ama’oy.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Endaho o biby hako am-bindao, o añombelahy maroo rekets’ o dronga’ ondatioo, songa mandialia tseram-bolafoty; navarakai’e ondaty tea alio.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Hiavotse e Mitsraime ao o sorotà’eo, halisa hañity fitàñe aman’Añahare t’i Kose.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
Misaboa aman’Andrianañahare, ry fifehea’ ty tane toio; rengeo an-tsabo t’i Talè; Selà
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
I miningitse andindì’ o likerañe haehaeo, Inay, ampionjone’e i fiarañanaña’ey, i fiarañanañañe ra’elahiy.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Iantofo te an’Andrianañahare ty haozarañe ambone’ Israele eo ty ahe’e an-dikerañe ao ty hafatrara’e.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Mampañeven-drehe, ry Andrianañahare, an-toe’o miavake ao; I Andrianañahare’ Israele, ro mpanolotse haozarañe naho hafatrarañe am’ondati’eo. Andriañeñe t’i Andrianañahare!

< Zaburi 68 >