< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
Au maître-chantre. — Psaume de David. — Cantique. Que Dieu se lève, et ses ennemis seront dispersés; Ceux qui le haïssent fuiront devant sa face; ,
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Comme la fumée se dissipe, tu les dissiperas; Comme la cire fond au feu, Ainsi périront les méchants devant Dieu.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
Mais les justes se réjouiront; Ils triompheront en présence de Dieu; Ils seront transportés d'allégresse.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Chantez à la gloire de Dieu, célébrez son nom. Préparez le chemin A celui dont le char s'avance à travers les plaines! L'Éternel est son nom; réjouissez-vous en sa présence!
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Il est le père des orphelins et le défenseur des veuves, Le Dieu qui réside dans sa demeure sainte.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
Dieu donne un foyer aux isolés; Il délivre les captifs et les met dans l'abondance; Mais les rebelles auront pour séjour le désert aride.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
Dieu, quand tu sortis à la tête de ton peuple, Quand tu t'avanças dans le désert. (Pause)
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
La terre trembla, les cieux se fondirent devant Dieu; Le Sinaï même trembla devant Dieu, le Dieu d'Israël.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
Tu fis tomber, ô Dieu, une pluie de bienfaits sur ton héritage: Il était épuisé; tu restauras ses forces.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Ton troupeau habita dans ce pays. Que dans ta bonté, ô Dieu, tu avais préparé pour le malheureux.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
Le Seigneur donne un ordre. Aussitôt les messagères de bonnes nouvelles Se réunissent en une troupe nombreuse.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Les rois des armées s'enfuient; ils s'enfuient. Et celle qui gardait la maison partage le butin.
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
Tandis que vous reposez au milieu des bercails. Les ailes de la colombe se couvrent d'argent, Et son plumage de reflets d'or.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Quand le Tout-Puissant dispersa les rois, Il y eut sur le Tsalmon comme des flocons de neige.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
Montagnes de Dieu, montagnes de Basan, Montagnes aux cimes nombreuses, montagnes de Basan,
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Montagnes aux cimes nombreuses, Pourquoi êtes-vous jalouses De la montagne que Dieu a choisie pour demeure? Oui, l'Éternel y demeurera toujours.
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Les chars de Dieu se comptent par vingt mille. Par milliers de milliers. Le Seigneur vient du Sinaï dans son sanctuaire.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Tu es monté sur la hauteur, tu as emmené des captifs; Tu as reçu les dons des hommes, même ceux des rebelles, Pour établir là ta demeure, ô Éternel Dieu!
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Béni soit le Seigneur! Chaque jour il porte nos fardeaux, Le Dieu de notre salut. (Pause)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Dieu est pour nous le Dieu qui nous sauve; C'est l'Éternel, le Seigneur, qui délivre de la mort.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
Oui, Dieu écrasera la tête de ses ennemis. Le crâne chevelu de celui qui se plaît à marcher dans le crime.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
Le Seigneur a dit: «De Basan je ramènerai mon peuple. Je le ramènerai des profondeurs de la mer,
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
Afin que tu plonges tes pieds dans le sang, Et que la langue de tes chiens ait part Au carnage de l'ennemi!»
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
On a vu ta marche, ô Dieu, La marche de mon Dieu, de mon Roi, dans le sanctuaire.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
En tête venaient les chanteurs; En arrière, les joueurs d'instruments; Au milieu, les jeunes filles battant du tambourin.
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
Bénissez Dieu dans vos assemblées; Bénissez le Seigneur, vous, descendants d'Israël!
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
Voici Benjamin, le plus jeune, qui marche en tête; Puis, les princes de Juda et leur troupe. Les princes de Zabulon et les princes de Nephthali.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Ton Dieu a décrété ta puissance. Affermis, ô Dieu, ce que tu as fait pour nous,
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
Du haut de ton palais qui domine Jérusalem! Que les rois t'offrent des présents!
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Tance la bête des roseaux, La troupe des taureaux Qu'entoure la multitude de leurs vassaux, Afin que tous se prosternent en t'offrant des lingots d'argent. Disperse les peuples qui veulent la guerre.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Les grands viendront de l'Egypte; L'Ethiopie s'empressera de tendre les mains vers Dieu.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
Royaumes de la terre, chantez un cantique à la gloire de Dieu! (Pause) Chantez en l'honneur du Seigneur,
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
En l'honneur de celui qui s'avance. Porté sur les cieux, les cieux éternels! Il fait retentir sa voix, sa voix puissante.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Rendez hommage à Dieu! Sa majesté resplendit sur Israël; sa force éclate dans les nuées.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Dieu, du fond de tes sanctuaires, tu te rends redoutable! C'est lui, le Dieu d'Israël, Qui donne force et puissance à son peuple. Béni soit Dieu!

< Zaburi 68 >