< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
Jusqu'à la Fin, psaume de David, Que Dieu se lève, et que ses ennemis soient dispersés; que ceux qui le haïssent s'enfuient loin de sa face.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Qu'ils s'évanouissent comme s'évanouit la fumée; que les pécheurs, devant la face de Dieu, périssent, comme fond la cire devant le feu.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
Que les justes se réjouissent, qu'ils tressaillent devant Dieu; qu'ils soient dans la joie et les délices.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Chantez à Dieu, chantez des louanges à son nom; faites une voie pour celui qui monte vers l'Occident: le Seigneur est son nom, tressaillez en sa présence. Ils seront troublés devant la face de celui
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Qui est le père des orphelins et le juge des veuves; tel est Dieu en son lieu saint.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
Dieu fait habiter en sa demeure ceux d'un même vouloir; il délivre les esclaves de la chair, même ceux qui l'irritent et qui habitent des sépulcres.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
Dieu, quand tu marchais devant ton peuple, quand tu traversais le désert,
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
La terre trembla, et les cieux versèrent de l'eau devant le Dieu du Sina, devant le Dieu d'Israël.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
O Dieu, tu réserves pour ton héritage une pluie venant de ta grâce; car il languissait, et tu l'as raffermi.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Tes animaux y habiteront; en ta bonté, ô Dieu, tu as préparé ce qu'il faut à l'indigent.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
Le Seigneur accordera le don de sa parole avec une grande puissance à ceux qui annonceront la bonne nouvelle.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Le roi des armées du peuple bien-aimé et choisi partagera les dépouilles à la beauté de sa maison.
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
Si vous avez votre couche au milieu des lots, vos ailes seront argentées comme celles de la colombe, et votre dos brillera de la couleur vert et or.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Tandis que le roi céleste dispersera les rois en sa terre, ils seront blancs comme la neige de Selmon.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
La montagne de Dieu est une montagne grasse, une montagne d'abondance, une montagne fertile.
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Pourquoi vous défiez-vous des grasses montagnes du Seigneur? C'est la montagne où il a plu à Dieu de résider; car le Seigneur y aura éternellement son tabernacle.
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
Le char de Dieu contient une myriade, des milliers de bienheureux; le Seigneur est avec eux en Sina, dans le lieu saint.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
Monté en haut, tu as emmené des captifs; tu as reçu des présents pour les hommes, même pour abriter des infidèles.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Béni soit le Seigneur Dieu; béni soit chaque jour le Seigneur; et le Dieu de notre salut nous fera prospérer dans notre voie.
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Notre Dieu est le Dieu du salut, et au Seigneur appartiennent les fins de la mort.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
Toutefois Dieu brisera la tête de ses ennemis; il ôtera la couronne des cheveux de ceux qui cheminent en leurs péchés.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
Le Seigneur a dit à son peuple: Je te ramènerai de Basan, je te ramènerai du fond de la mer;
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
Afin que ton pied se baigne dans le sang, et la langue de tes chiens dans le sang des ennemis de Dieu.
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
Ils ont vu ta marche, ô Dieu, la marche de mon Dieu, du Roi qui est en son lieu saint.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
Et les princes, joints aux chanteurs, ont pris l'avance au milieu des jeunes filles frappant des tambours, et chantant:
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
Bénissez Dieu dans les églises; bénissez le Seigneur des fontaines d'Israël.
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
Là Benjamin, le plus jeune des fils de Jacob, est en extase; là sont les princes de Juda, les princes de Zabulon, les princes de Nephthali.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
Dieu, commande à ta force: confirme, ô Dieu, ce que tu as ordonné en nous!
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
A cause de ton temple de Jérusalem, des rois t'apporteront leurs présents.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Châtie les bêtes fauves des roseaux; châtie ces taureaux assemblés contre les génisses des peuples, afin que ceux qui ont été éprouvés, comme de l'argent, ne soient point exclus. Disperse les nations qui veulent la guerre.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Des anciens viendront de l'Égypte; l'Éthiopie sera la première à étendre les mains vers Dieu.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
O vous, royaumes de la terre, chantez à Dieu, chantez des psaumes au Seigneur, chantez à Dieu,
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
Qui est monté sur le ciel des cieux vers l'Orient; voilà qu'il va faire entendre le son puissant de sa voix.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Rendez gloire à Dieu; sa magnificence est sur Israël, et sa puissance dans les nuées.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
Dieu est admirable dans ses saints; le Dieu d'Israël donnera lui-même la force à son peuple et l'affermira; béni soit Dieu!

< Zaburi 68 >