< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
God, arise and scatter your enemies, and cause those who hate you to run away from you.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
Like [wind] blows smoke away, chase your enemies away. Like wax melts when it is near a fire, cause wicked people to (disappear/be destroyed).
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
But righteous people should be joyful; they should rejoice when they are in God’s presence; they should be happy, and be very joyful.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Sing to God; sing to praise him; sing a song (OR, make a road) for him who rides on the clouds; his name is Yahweh; be glad when you are in his presence.
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
God, who lives in his sacred temple, is [like] [MET] a father to [those who are] orphans, and he is the one who protects widows.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
For those who have no one to live with, he provides families [to live with]. He frees prisoners and enables them to be successful, but those who rebel [against him] will be forced to live in a very hot and dry land.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
God, you led your people out [of Egypt], and then you marched with them through the desert.
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
After you did that, because when you, the God [worshiped by us] Israeli people, appeared to us at Sinai [Mountain], the earth shook, and rain poured down from the sky.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
You caused plenty of rain to fall [on your land], [and so] you enabled good crops to grow again on the land that you gave [to us Israelis].
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Your people built homes there; and because you were good to them, you provided [food] for those who were poor.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
The Lord gave a message, and many women took that message to other places.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
[They proclaimed], “Many kings and their armies are running away [from our army]!” [When our army brought back to their homes] the things that they captured, the women who were at home divided up those things [among themselves and among their families].
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
Even those women who were in the pens [taking care of] the sheep [received some of those things]; they got statues of doves whose wings were covered with silver and whose feathers were covered with pure yellow gold.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
When Almighty [God] scattered the [enemy] kings [and their armies], [the number of weapons that they abandoned there] seemed like there had been a snowstorm on Zalmon (OR, a black) [Mountain].
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
There is a very high mountain in the Bashan [region], a mountain which has many peaks.
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
But the [people who live near] that mountain should not [RHQ] envy those who live near [Zion], the mountain on which God chose to live! Yahweh will live there forever!
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
[After we defeated all our enemies], [it was as though] the Lord, surrounded by many thousands of strong chariots, descended from Sinai [Mountain] and came into the sacred temple [in Jerusalem].
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
He ascended the sacred mountain [where his temple is], and took with him many people who had been captured [in battles]; and received gifts from the enemies [whom he had defeated]. He received gifts even from those who had rebelled against him, and Yahweh our God will live there [in his sacred temple] forever.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Praise the Lord, who [helps us] carry our heavy loads every day; he is the one who saves/rescues us.
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
Our God is the God who saves us; He is Yahweh, our Lord, the one who (allows us to escape/prevents us) from being killed [in battles].
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
But God will smash the heads of his enemies, the skulls of those who continue to behave sinfully.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
The Lord said, “I will bring back the [corpses of those who were killed in] Bashan, and I will bring back those who sank deep in the ocean [and drowned].
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
I will do that in order that you may wash your feet in their blood, and your dogs can [also] lap up some of your enemies’ blood.”
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
God, many people see you march triumphantly into your sacred temple, [celebrating that you have defeated your enemies]. You [march like] a king does, and a large crowd walks with you.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
The singers are in front, and the people who play stringed instruments are at the rear, and young women who are beating their tambourines are between them.
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
[They are all singing], “You Israeli people, praise God when you gather together; praise Yahweh, all you who are descendants of Jacob!”
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
First come [the people of the tribe of] Benjamin, the smallest [tribe], and following them come the leaders of [the tribe of] Judah and their group, and following them come the leaders of [the tribes of] Zebulun and Naphtali.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
God, show people that you are very powerful; show people the power with which you have helped us previously.
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
Show that power from your temple in Jerusalem, where kings bring gifts to you.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Rebuke [your enemies, such as those in Egypt who are like] wild hippopotamuses/animals that live in the reeds; and [powerful nations that are like] bulls that are among their calves [MET]; rebuke/trample them until they bow down and give you gifts of silver. Scatter the people who enjoy making wars.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
Then people will bring gifts of bronze (OR, of cloth) to you from Egypt; the people in Ethiopia will lift up their hands [to praise you].
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
[You people who are citizens of] kingdoms/countries all over the world, sing to God! Sing praises to the Lord!
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
Sing to the God, the one who rides across the sky, the sky that [he created] long ago. Listen as he shouts with a very powerful voice.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Proclaim that God is very powerful; he is the king that rules over Israel, and in the skies [he also shows that] he is powerful.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
God is awesome as he comes out of his sacred temple; he is the God whom [we] Israeli people [worship]. He makes [DOU] his people very powerful. Praise God!

< Zaburi 68 >